NYOTA wa Brazil, Neymar anaamini timu yake itashinda Kombe la Dunia bila ya kuwa na yeye.

Mchezaji huyo wa Barcelona aliaga mashineano hayo juzi usiku baada ya kuchezewa rafu na mchezaji wa Colombia, Juan Zuniga.
Mchezaji huyo ameelezea maumivu yake baada ya pogo hilo linalomuondoa Kombe la Dunia mapema akiiacha timu yake imetinga Nusu Fainali- na zaidi amewatakia heri wachezaji wenzake wabakize nyumbani.
Neymar amesafirishwa kwa helikopta baada ya tiba ya awali kupelekwa Sao Paulo kuanza mapumziko. Tayari FIFA imesema inalifanyia uchunguzi tukio hilo kabla ya kumchukulia hatua Zuniga.
Anaondoka: Neymar amesafirishwa kwa helikopta kupelekwa Sao Paulo kuanza mapumziko

Neymar amesema bado anaweza kushangilia Kombe la Dunia na wachezaji wenzake mjini Rio

Safari njema: Neymar akipewa pole na Rais wa Shirikisho la Soka Brazil, Jose Maria Marin



.png)
0 comments:
Post a Comment