STRAIKA wa zamani wa Sunderland na timu ya taifa ya Uskochi, Kevin Kyle amekuwa akikidhi mahitaji ya familia yake kwa kufanya kazi kama mtunza stoo katika meli moja kwenye visiwa vya Shetland.
Kyle, ambaye amewahi kucheza mechi 10 kwenye timu ya taifa ya nchi yake, aliachana na klabu yake ya mwisho ya Ayr United mapema mwaka huu na kwa sasa anafanya kazi masaa 12 katika meli ya Regina Baltica huko Lerwick.
Meli hiyo inatumika kwa hoteli inayoelea kwenye maji kwa wafanyakazi wanaofanya kazi kwenye viwanda vya mafuta kwa mujibu wa rekodi za kila siku Kyle anafanya kazi ya kusafisha meli hiyo, kutandika vitanda na kuweka vitu stoo.
Kyle, ambaye amewahi kucheza mechi 10 kwenye timu ya taifa ya nchi yake, aliachana na klabu yake ya mwisho ya Ayr United mapema mwaka huu na kwa sasa anafanya kazi masaa 12 katika meli ya Regina Baltica huko Lerwick.
Meli hiyo inatumika kwa hoteli inayoelea kwenye maji kwa wafanyakazi wanaofanya kazi kwenye viwanda vya mafuta kwa mujibu wa rekodi za kila siku Kyle anafanya kazi ya kusafisha meli hiyo, kutandika vitanda na kuweka vitu stoo.


Straika: Akiwa na urefu wa futi 6 na inch 3, Kyle alikuwa akisifika kwa kucheza mipira ya vichwa

Furaha: Kevin Kyle akishangilia baada ya kufunga bao akiwa na kikosi cha Sunderland, Mei 2004
Alipoulizwa na Daily Record kuhusu kazi yake inayomuingizia pauni 800 kwa wiki mbili, Kyle mwenye umri wa miaka 33 alisema; “Najaribu kuikimu familia yangu.”
Kyle alianza kucheza soka katika klabu ya Sunderland mwaka 2000, ambako aliichezea katika mechi 39 za Ligi Kuu England na kufunga mara moja.
Aliichezea Uskochi mechi yake ya kwanza mwaka 2002 na kuifungia nchi yake mara moja.
Aliichezea klabu za Coventry (ilimlipia pauni 600,000 kutoka Sunderland mwaka 2006), Kilmarnock, Hearts na Rangers pamoja na timu kadhaa zingine kwa mkopo kabla ya kuhamia Ayr United, ambako mara ya mwisho alichezea Januari.
Kyle bado hajatundika daluga rasmi, lakini amekosa klabu ya kuchezea tangu aondoke Ayr United.
Mzaliwa huyo wa Stranraer ambaye zamani ameathiriwa na matatizo ya kucheza kamari, kiasi cha kutumia pauni 7,000 kwa wiki kwenye kamari. Amekuwa akitumia muda wake wa ziada kuwaambia wachezaji vijana athari za kuendekeza kucheza kamari.
Kwenye kilele cha mafanikio yake ya soka Kyle alikuwa akilipwa pauni 10,000 kwa wiki yaani kwa siku aliingiza fedha nyingi kuliko zile ambazo anangiza sasa kwa wiki mbili.
Kyle alianza kucheza soka katika klabu ya Sunderland mwaka 2000, ambako aliichezea katika mechi 39 za Ligi Kuu England na kufunga mara moja.
Aliichezea Uskochi mechi yake ya kwanza mwaka 2002 na kuifungia nchi yake mara moja.
Aliichezea klabu za Coventry (ilimlipia pauni 600,000 kutoka Sunderland mwaka 2006), Kilmarnock, Hearts na Rangers pamoja na timu kadhaa zingine kwa mkopo kabla ya kuhamia Ayr United, ambako mara ya mwisho alichezea Januari.
Kyle bado hajatundika daluga rasmi, lakini amekosa klabu ya kuchezea tangu aondoke Ayr United.
Mzaliwa huyo wa Stranraer ambaye zamani ameathiriwa na matatizo ya kucheza kamari, kiasi cha kutumia pauni 7,000 kwa wiki kwenye kamari. Amekuwa akitumia muda wake wa ziada kuwaambia wachezaji vijana athari za kuendekeza kucheza kamari.
Kwenye kilele cha mafanikio yake ya soka Kyle alikuwa akilipwa pauni 10,000 kwa wiki yaani kwa siku aliingiza fedha nyingi kuliko zile ambazo anangiza sasa kwa wiki mbili.


Hana mkataba: Kyle hajatundika daluga rasmi kutoka kwenye soka lakini amekuwa hana timu tangu Januari

Heshima ya kimataifa: Kyle akiruka kichwa wakati akiichezea Scotland dhidi ya Denmark, Agosti 2002

Tatizo la Majeruhi: Miaka miwili ya Kyle katika klabu ya Hearts kati ya 2010 hadi 2012 ilitawaliwa na majeruhi
WASIFU WA KEVIN KYLE:
Sunderland (2000-06), Huddersfield (2000)*, Darlington (2000-01)*, Rochdale (2001)*, Coventry (2006-09), Wolves (2008)*, Hartlepool (2008)*, Kilmarnock (2009-10), Hearts (2010-12), Rangers (2012-13), Ayr United (2013-14). Scotland (2002-10)
Jumla: Mechi 320, mabao 69.
* Inahusiaha timu alizocheza kwa mkopo
Jumla: Mechi 320, mabao 69.
* Inahusiaha timu alizocheza kwa mkopo
Kyle alicheza kwa kipindi kifupi Rangers katika msimu wa 2012-13 na anakiri kushtushwa na fedha ambazo wachezaji walikuwa wakipata kwenye klabu hiyo ambayo ilikuwa na matatizo ya fedha.
Alisema: “Kuna wachezaji pale Rangers ambao hawawezi kuamini jinsi gani wanabahati kwa kile wanachokiingiza.
“Nilimuuliza mchezaji mwenzangu wakati wa kiangazi, ‘Kweli Rangers wamekupa ofa ya kiasi hicho cha fedha?”
“Alinijibu, “Unajua nini? Nadhani ninaweza kuwakamua zaidi.”
Alisema: “Kuna wachezaji pale Rangers ambao hawawezi kuamini jinsi gani wanabahati kwa kile wanachokiingiza.
“Nilimuuliza mchezaji mwenzangu wakati wa kiangazi, ‘Kweli Rangers wamekupa ofa ya kiasi hicho cha fedha?”
“Alinijibu, “Unajua nini? Nadhani ninaweza kuwakamua zaidi.”




.png)
0 comments:
Post a Comment