• HABARI MPYA

    Sunday, August 11, 2013

    RONALDO KAMA ANARUDI MAN UNITED HIVI...SASA JEZI NAMBA 7 KAWEKEWA NANI KAMA SI YEYE?

    IMEWEKWA AGOSTI 11, 2013 SAA 2:08 USIKU
    MANCHESTER United imeweka jezi namba saba maalum kwa ajili ya Cristiano Ronaldo atakaporejea Old Trafford? David Moyes anajua.
    Real Madrid imesema kwamba winga huyo wa zamani wa Manchester United hauzwi, na katika taarifa siyo rasmi, gazeti la kila siku la Hispania, Marca, hivi karibuni limetoa habari ukurasa wa mbele, ikisema ameongeza Mkataba mrefu wa kuendelea kupiga kazi Bernabeu.
    Lakini hiyo haiwezi kumzuia Moyes kumuwekwa Ronaldo jezi yake aliyokuwa akivaa akiwa Manchester, namba saba (7) ikiwa haina jina wakati United ilipotambulisha kikosi chake cha msimu mpya.
    Debut: Ronaldo wears the No 7 for the first time against Bolton
    Mwanzoni: Ronaldo alivaa jezi namba saba (7) kwa mara ya kwanza katika mechi dhidi ya Bolton
    Adored: Rio Ferdinand celebrates with Ronaldo
    Rio Ferdinand akishangilia na Ronaldo
    Deadly: Ronaldo scores United's third goal in their Carling Cup final victory over Wigan in 2006
    Ronaldo aliifungia United bao la tatu katika fainali ya Kombe la Ligi, maarufu kama Carling dhidi ya Wigan mwaka 2006

    Antonio Valencia aliyekuwa anavaa jezi hiyo msimu uliopita sasa amehamia jezi namba 25.
    Na ikiwa hajatajwa mtu mpya wa kuvaa jezi hiyo, ambayo awali ilipata umaarufu kupitia George Best, Moyes anaachwa maswali vichwani mwa mashabiki wa timu hiyo- kwamba huenda amemuachia Ronaldo aliyetimkia Madrid kwa dau la rekodi ya dunia.
    Hero: Ronaldo gives thumbs up to the United faithful
    Shujaa: Ronaldo alifanya vizuri enzi zake United
    Ronaldo celebrates a goal for Portugal with team-mate Miguel Veloso
    Ronaldo akishangilia bao na mchezaji mwenzake wa Ureno, Miguel Veloso
    The former United star also sports No 7 for current side Real Madrid
    Nyota wa zamani wa United ameendelea kuvaa jezi namba saba (7) hata katika klabu yake ya sasa, Real Madrid
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: RONALDO KAMA ANARUDI MAN UNITED HIVI...SASA JEZI NAMBA 7 KAWEKEWA NANI KAMA SI YEYE? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top