IMEWEKWA AGOSTI 24, 2013 SAA 3:57 ASUBUHI
KOCHA David Moyes anakaribia kushinda vita yake ya kuwania saini za wachezaji wa Everton, Leighton Baines na Marouane Fellaini baada ya kuibuka kwa taarifa kwamba, klabu yake ya zamani iko tayari kuwauza nyota wake hao.
Everton imekuwa ikilalama dhidi ya Moyes na Manchester United tangu ikatae ofa ya mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England ya Pauni Milioni 28 kwa ajili ya nyota hao wawili wa Goodison Park.
Wamekubaliana na ofa hiyo na kocha wa Everton, Roberto Martinez ameisifu United imekuwa na tabia nzuri.
Nakuja kwako: David Moyes anakaribia kuwanasa wachezaji wake wa zamani Leighton Baines na Marouane Fellaini
Anaonekana vizuri: Baines akiwa mazoezini na Everton
Anabaki au anaondoka? Fellaini (kulia) na Baines mazoezini na Everton kujiandaa na mchezo dhidi ya West Brom