IMEWEKWA AGOSTI 22, 2013 SAA 12:32 ASUBUHI
KOCHA Jose Mourinho ameendelea kutamba katika Ligi Kuu ya England kufuatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Aston Villa.
Kwanza, kocha huyo wa Chelsea alitikiswa kwa bao la kusawazisha la Christian Benteke na kisha akavaana na kocha wa Aston Villa, Paul Lambert.
Mourinho anafahamu Chelsea ilibahatika. Wameshinda wakati Branislav Ivanovic, ambaye angepewa kadi nyekundu kiulaini kwa kumchezea rafu Benteke, kufunga bao la ushindi.
Luna alitangulia kuifungia Chelsea dakika ya saba kabla ya Benteke kusawazisha dakika ya 45 na Ivanovic akafunga la ushindi dakika ya 73.
Kikosi cha Chelsea kilikuwa: Cech, Ivanovic, Cahill, Terry, Cole, Ramires, Lampard, Oscar/Van Ginkel dk84, Mata/Schurrle dk65, Hazard na Ba/Lukaku dk65.
Aston Villa: Guzan, Lowton, Vlaar, Clark/Okore dk43, Luna, El Ahmadi/Tonev dk82, Westwood, Delph, Weimann, Benteke na Agbonlahor.
Gonga HAPA matokeo zaidi, msimamo na ratiba Ligi Kuu England

Pointi tatu: Chelsea wakishangilia baada ya kushinda 2-1 jana

Ivanovic akifunga bo la ushindi

Jose Mourinho akizinguana na kocha mpinzani wake, Paul Lambert

Hakuna furaha: Ugomzi ulitokana na rafu ya Ivanovic kwa Christian Benteke

Refa wa akiba akijaribu kuwasuluhisha

Lambert akijibu mapigo

Ivanovic akimchezea rafu Christian Benteke, lakini akapewa kadi ya njano tu

Benteke akishika uso wake baada ya rafu ya Ivanovic

Chelsea ilipata bao la mapema baada ya shutila Eden Hazard kumfanya Antonio Luna ajifunge.
Jinsi Luna alivyojifunga na kuipa Chelsea pointi tatu- gonga kupata zaidi yaliyojiri Stamford Bridge


Benteke akishangilia bao lake

Kocha wa Villa, Lambert akiruka kushangilia bao la Benteke

Demba Ba akipambana na Jores Okore

Eden Hazard alitoa mchango mkubwa kwa bao la kwanza la Chelsea

Beki wa Villa, Demba Ba akipambana kabla ya kutolewa

Ciaran Clark akitokwa damu

Ramires na Fabian Delph wakipambana


.png)