IMEWEKWA AGOSTI 19, 2013 SAA 6:48 MCHANA
KLABU ya Everton imekataa ofa ya Pauni Milioni 28 kutoka Manchester United kwa ajili ya kuwanunua Leighton Baines na Marouane Fellaini.
United imejaribu kumnunua kwa Pauni Milioni 16 Fellaini - baada ya kukwama kuwanunua wachezaji wote kwa Pauni Milioni 23.5 na kisha inajaribu pia kumnunua Baines kwa Pauni Milioni 12, kwa mujibu wa gazeti la Liverpool, Echo.
Si ajabu, Everton imeipiga chini ofa hiyo mara moja kutoka kwa kocha wao wa zamani, David Moyes, ambayo ilipelekwa siku mbili kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu England.
Wawili kwa mpigo: Kocha wa Manchester United, David Moyes (chini) anajaribu kuwasajili wachezaji wa klabu yake ya zamani, Everton, Marouane Fellaini (kushoto) na Leighton Baines (kulia) wote kwa Pauni Milioni 28- lakini klabu ya Merseyside imepiga chini ofa hiyo.
Ikiwa imekwama kuzinasa saini za Cesc Fabregas, Thiago Alcantara na wachezaji wengine iliyowahitaji majira haya ya joto, United sasa imeelekeza nguvu zake kwa wawili hao wa Everton kuimarisha kikosi chake.
Lakini ofa kwa Fellaini na Baines imeripotiwa kuwa chini ya thamani ya mchezaji huyo kwa kiasi cha Pauni Milioni 10 ambayo Everton wanataka.
Sasa Moyes, aliyerithi mikoba ya Sir Alex Ferguson Juni, mwaka huu atatakiwa kujipanga upya.
Wamerudi kazini: Wote Baines (kushoto) na Fellaini waliichezea Everton dhidi ya Norwich City katika sare ya 2-2 Uwanja wa Carrow Road Jumamosi