• HABARI MPYA

    Wednesday, August 21, 2013

    ARSENAL YATAKA KUMSAJILI IKER CASILLAS WA REAL MADRID, ILA KWA UBAKHILI WAO WATAMKOSA

    IMEWEKWA AGOSTI 21, 2013 SAA 6:45 MCHANA
    KLABU ya Arsenal inataka kumsajili kipa wa Real Madrid, Iker Casillas ili akawe mbadala wa anayefanya madudu kwa sasa, Wojciech Szczesny. 
    Nahodha huyo wa Hispania inafahamika hajatulia Bernabeu, baada ya kupoteza nafasi ya kuwa kipa wa kwanza wa klabu chini ya kocha Jose Mourinho aliyehamia Chelsea na The Gunners inamfuatilia kwa makini. 
    Arsenal - ilipigwa mshituko katika mechi yao ya ufunguzi ya Ligi Kuu ya England kwa kufungwa 3-1 na Aston Villa - sasa ninataka kusajili kipa wa kiwango cha duni na mshindi huyo wa Kombe la Dunia na Ubingwa wa Ulaya anaweza kuwa sawa yao. 
    London calling? Real Madrid goalkeeper Iker Casillas is a target for Arsenal manager Arsene Wenger
    London inamuita? Kipa wa Real Madrid, Iker Casillas anatakiwa na kocha wa Arsenal, Arsene Wenger
    Benched: Casillas lost his place in the Real Madrid team under Jose Mourinho and has yet to win it back
    Benchi: Casillas amepoteza nafasi ya kipa wa kwanza Real Madrid tangu chini ya Jose Mourinho na hajafanikiwa kurejesha nafasi hiyo
    In action: Casillas (left) stops a shot from Manchester City's Sergio Aguero in the Champions League last season
    Kazini: Casillas (kushoto) akizuia mchomo wa Sergio Aguero katika Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita
    Leading man: Casillas (centre) lifts the Euro 2012 trophy as Spain captain
    Kiongozi: Casillas (katikati) akiinua Kombe la Euro 2012 akiwa Nahodha wa Hispania
    Iker Casillas
    Iker Casillas
    Mfalme wa Dunia: Casillas akiinua Kombe la Dunia (kushoto) na kulia taji la kwanza la Euro kwa Hispania mwaka 2008
    Klabu hiyo ya London Kaskazini ilijadili uwezekano wa kumsajili kipa wa kwanza wa Chelsea, Petr Cech kabla ya kufunguliwa kwa pazia la usajili, ikiamini kwamba Thibaut Courtois atarejea kutoka Atletico Madrid alikokuwa akicheza kwa mkopo na kuchukua nafasi ya Cech Stamford Bridge. 
    Arsene Wenger pia anamtolea macho Casilllas, kipa ambaye anaamini ataendana na bei yake. Casillas ana miaka 32 na kwa kuwa Arsenal haitaki kutoa fedha nyingi itakuwa vigumu kumpata. 
    Wanaweza kufikiria kutoa ada ya kiasi cha Pauni Milioni 8, lakini kwa Madrid haiwezi kusikiliza ofa ya chini ya Pauni Milioni 15.
    Struggling: Arsenal's current No 1 Wojciech Szczesny saw Aston Villa score three past him on Saturday
    Anatunguliwa tu: Kipa wa kwanza wa sasa wa Arsenal, Wojciech Szczesny alishuhudiwa akitunguliwa mabao matatu na Aston Villa Jumamosi
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ARSENAL YATAKA KUMSAJILI IKER CASILLAS WA REAL MADRID, ILA KWA UBAKHILI WAO WATAMKOSA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top