• HABARI MPYA

    Tuesday, August 27, 2013

    MAZOEZI YA MWISHO AZAM FC KABLA YA KUIVAA RHINO KESHO, BOCCO NJE, KARIHE NA NYONI 'TIA TIA MAJI'

    IMEWEKWA AGOSTI 27, 2013 SAA 11:48 JIONI
    Kocha Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart John Hall akimpa maelekezo mchezaji wake, kiungo Khamis Mcha 'Vialli' kwenye Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora jioni ya leo. Azam itamenyana na wenyeji Rhino Rangers kesho kwenye Uwanja huo katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. 

    Mshambuliaji Seif Abdallah Karihe akitibiwa na daktari wa timu, Vincent Madege baada ya kuumia kifundo cha mguu mazoezini leo

    Beki Erasto Nyoni akipewa mazoezi mepesi na Dk, Madege leo

    Kikao cha dharula; Kocha Stewart Hall akijadiliana na wasaidizi wake Ibrahim Shikanda kulia na Kali Ongala kushoto wakati wa mazoezi leo

    Beki Agrey Morris kulia akimtoka mshambuliaji Kipre Tchetche mazoezini leo

    Beki David Mwantika akimtoka Khamis Mcha Vialli nyuma yake. Wengine nyuma ni Waziri Salum na kulia ni Jabir Aziz

    Injini ya timu; Salum Abubakar 'Sure Boy' yuko fiti kabisa kwa mchezo wa kesho

    Mlinzi Mkuu; Beki wa kati Aggrey Morris yuko tayari kwa shughuli ya maafande wa JWTZ kesho

    Jabir Aziz kushoto akiwania mpira na Mudathir Yahya

    Kocha Msaidizi, Kali Ongala alishiriki mazoezi 

    John Bocco 'Adebayor' alikuwa nje kabisa akipiga stori na Meneja Jemadari Said kwa sababu ya maumivu

    Himid Mao akijimwagia maji mazoezini leo

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MAZOEZI YA MWISHO AZAM FC KABLA YA KUIVAA RHINO KESHO, BOCCO NJE, KARIHE NA NYONI 'TIA TIA MAJI' Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top