IMEWEKWA AGOSTI 22, 2013 SAA 12:00 ASUBUHI
KLABU ya Arsenal sasa imegeuzia mawindo wake kwa mshambuliaji wa Real Madrid, Karim Benzema katika harakati zake za kusaka mshambuliaji mpya chaguo la kwanza.
Licha ya ukweli kwamba Real Madrid ina washambuliaji wachache wa kati, lakini kocha Carlo Ancelotti anaweza kumuuza mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ufaransa.
Na klabu hiyo ya London Kaskazini imefanya mjadala mzito juu ya kumsajili mshambuliaji huyo.
Anatakiwa: Mshambuliaji wa Real Madrid, Karim Benzema (kulia) anatakiwa na kocha wa Arsenal, Arsene Wenger
Kocha Arsene Wenger anamzimikia kwa muda mrefu Benzema ana amejaribu kumsajili mshambuliaji huyo mara kadhaa bila mafanikio.
Lakini Arsenal sasa wanaonekana kuwa katika nafasi nzuri ya kumnasa mshambuliaji huyo kabla ya kufungwa kwa pazia la usajili Septemba 2.
Wenger amepagawa mno baada ya kuwakosa washambuliaji aliokuwa anawataka Luis Suarez na Wayne Rooney, lakini wakimpata Benzema watapunguza matatizo.
Anafunga: Benzema aliifungia Madrid dhidi ya Real Betis katika mchezo wa ufunguzi wa La Liga
Wamemkosa: Luis Suarez hatajiunga na Arsenal majira haya ya joto