• HABARI MPYA

    Friday, August 30, 2013

    ARSENAL NA BARCA KATIKA KUNDI LA KIFO LIGI YA MABINGWA

    Na Mwandishi Wetu, IMEWEKWA AGOSTI 30, 2013 SAA 10:00 USIKU
    MABINGWA mara saba wa Ulaya, AC Milan, waliotolewa na Barcelona katika Ligi ya Mabingwa misimu miwili iliyopita, wamepangwa kundi moja na vigogo hao wa Katalunya katika hatua ya makundi msimu huu baada ya droo iliyopangwa jana.
    Arsenal ambayo kocha wake Arsene Wenger anapambana kusajili jina kubwa kabla ya pazia kufungwa, imepangwa Kundi F pamoja na Marseille ya Ufaransa, Borussia Dortmund ya Ujerumani na Napoli ya Italia.
    Mabingwa mara tisa, Real Madrid wamepangwa kundi moja na Juventus, B ambalo pia lina timu za Galatasaray and FC Copenhagen.

    Mabingwa watetezi, Bayern Munich wamepangwa na CSKA Moscow, Manchester City na mabingwa wa Czech, Viktoria Plzen Kundi D, ambayo inawapa njia nyeupe ya kufuzu.
    Chelsea, mabingwa wa misimu miwili iliyopita, wamepangwa na Schalke 04, FC Basle na Steaua Bucharest Kundi E, timu mbili ambazo ilizifunga kuelekea kutwaa taji la Europa League msimu uliopita.
    Mabingwa mara tatu wa taji hilo, Manchester United imepangwa na Shakhtar Donetsk, Bayer Leverkusen na Real Sociedad katika Kundi A.
    AC Milan na Barcelona wamekutana mara sita katika misimu miwili iliyopita na Wakalunya wameng’ara dhidi ya Wataliano.

    KUNDI A

    Manchester United
    Shakhtar Donetsk
    Bayer Leverkusen
    Real Sociedad

    KUNDI B

    Real Madrid
    Juventus
    Galatasaray
    FC Copenhagen

    KUNDI C

    Benfica
    Paris Saint-Germain
    Olympiakos
    Anderlecht

    KUNDI D

    Bayern Munich
    CSKA Moscow
    Manchester City
    Viktoria Plzen

    KUNDI E

    Chelsea
    Schalke
    Basle
    Steaua Bucharest

    KUNDI F

    Arsenal
    Marseille
    Borussia Dortmund
    Napoli

    KUNDI G

    Porto
    Atletico Madrid
    Zenit St Petersburg
    Austria Vienna

    KUNDI H

    Barcelona
    AC Milan
    Ajax
    Celtic
    87 matches.jpg
    Timu ya Serie A ilifungwa mabao 4-2 jumla katika hatua ya 16 Bora mwaka jana na 3-1 jumla katika Robo Fainali misimu miwili iliyopita, wakati timu hizo zilipokutana pia kwenye hatua ya makundi.
    Timu hizo mbili zimepangwa katika Kundi H, sambamba na mabingwa mara nne Ajax Amsterdam na mabingwa wa 1967, Celtic, ambao walikutana na Barcelona katika hatua ya makundi msimu uliopita na kupata ushindi wa kukumbukwa wa nyumbani.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ARSENAL NA BARCA KATIKA KUNDI LA KIFO LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top