• HABARI MPYA

    Monday, August 12, 2013

    BOOM FC WAMPA ASANTE YAKE DK DAU NA NSSF

    Na Mohamed Mharizo, IMEWEKWA AGOSTI 12, 2013 SAA 1:14 ASUBUHI
    UONGOZI wa Boom FC umelishukuru Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwa kuipatia msaada wa Sh 5,125,000 kwa ajili ya uendeshaji wa timu hiyo katika Ligi Daraja la Pili Mkoa wa Dar es Salaam.
    Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Katibu mkuu wa Boom FC, Duni Mibavu amesema fedha hizo zitasaidia timu kufanya vizuri katika ligi na kuwapa morali wachezaji ili kuhakikisha timu hiyo inacheza Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao.
    Dk Ramadhani Dau

    “Tunawashukuru wenzetu wa NSSF chini ya Mkurugenzi wake Dk. Ramadhan Dau kwa msaada mkubwa walioutupatia, hii inaonyesha ni jinsi gani walivyoguswa na na kilio chetu na kuamua kutusaidia ili tufanye vizuri,” alisema.
    Duni ameomba na mashirika mengine pamoja na makampuni mbalimbali nayo kuiga mfano wa NSSF katika kuzisaidia timu za madaraja ya chini ili nazo zifanye vizuri
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: BOOM FC WAMPA ASANTE YAKE DK DAU NA NSSF Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top