• HABARI MPYA

    Wednesday, June 27, 2012

    SIMBA YAMTEMA RASMI JUMA JABU, HARUNA ATOLEWA KWA MKOPO


    Juma Jabu

    Na Prince Akbar
    KLABU tano za Ligi Kuu ya Tanzania zimewasilisha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) majina ya wachezaji ambao zimewakatishia mikataba/mikataba yao kumalizika au kuwaacha kwa ajili ya usajili wa wachezaji msimu wa 2012/2013.
    Kwa mujibu wa klabu hizo, wachezaji waliomaliza mikataba Simba kwa mujibu wa klabu hiyo ni Ally Mustafa, Derick Walulya, Gervais Kago, Juma Jabu wakati Salum Kanoni mkataba wake unatarajia kumalizika Juni 30 mwaka huu, wakati wachezaji ambao inakusudia kuwatoa kwa mkopo ni Rajab Isihaka, Salum Machaku, Haruna Shamte na Shija Mkina. 
    Polisi Morogoro iliyopanda msimu huu imeacha wachezaji 17 wakati Tanzania Prisons ambayo pia imepata hadhi ya Ligi Msimu huu imeacha wachezaji 11. Azam imekatisha mikataba ya wachezaji watatu.
    Wachezaji 12 wamemaliza mikataba yao katika klabu ya Kagera Sugar wakati wakati kwa upande wa Simba wachezaji waliomaliza mikataba ni wanne huku ikionesha nia ya kuwatoa kwa mkopo wengine wanne.
    Uhamisho wa wachezaji kwa msimu huu ulianza Juni 15 mwaka huu na utamalizika Julai 30 mwaka huu wakati kipindi cha kuanza wachezaji (kwa wasio wa Ligi Kuu) ni kati ya Juni 15 na 30 mwaka huu.
    Kwa klabu za Ligi Kuu kutangaza wachezaji watakaositishiwa mikataba yao ni kuanzia Juni 15-30 mwaka huu na usajili wa wachezaji unafanyika kuanzia Juni 15 hadi Agosti 10 mwaka huu.
    Wachezaji walioachwa Polisi Morogoro ni Abdul Ibadi, Ally Moshi, Benedict Kitangita, Hassan Kodo, Hussein Lutaweangu, Hussein Sheikh, Juma Maboga, Mafwimbo Lutty, Makungu Slim, Mbaraka Masenga, Method Andrew, Moses Mtitu, Ramadhan Kilumbanga, Ramadhan Toyoyo, Said Kawambwa, Salum Juma na Thobias John.
    Tanzania Prisons imewaacha Adam Mtumwa, Dickson Oswald, Exavery Mapunda, Ismail Selemani, Lwitiko Joseph, Mbega Daffa, Mwamba Mkumbwa, Musa Kidodo, Rajab Ally, Richard Mwakalinga na Sweetbert Ajiro.
    Wachezaji waliomaliza mikataba yao kwa mujibu wa Kagera Sugar ni Cassian Ponera, Hamis Msafiri, Hussein Swedi, Ibrahim Mamba, Martin Muganyizi, Mike Katende, Moses Musome, Msafiri Davo, Said Ahmed, Said Dilunga, Steven Mazanda na Yona Ndabila.
    Azam imewasitishia mikataba wachezaji Tumba Swedi, Mau Bofu na Sino Augustino. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA YAMTEMA RASMI JUMA JABU, HARUNA ATOLEWA KWA MKOPO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top