• HABARI MPYA

    Friday, June 29, 2012

    SIMBA KUANZA NA URA, YANGA NA WARUNDI KAGAME, AZAM WAPEWA WAZENJI


    Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholaus Musonye kulia akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi za TFF, mchana huu. Kushoto ni Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah.

    Na Prince Akbar
    MABINGWA watetezi wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame watafungua dimba na Atletico ya Burundi katika mchezo wa Kundi C wa michuano hiyo, Julai 14, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati wapinzani wao wa jadi, Simba SC waliowekwa Kundi A, wataanza na URA ya Uganda Julai 16, kwenye Uwanja huo huo.
    Wawakilishi wengine wa Tanzania katika michuano hiyo, Azam FC wao wataanza na Mafunzo ya Zanzibar katika mchezo wa Kundi B, Uwanja wa Chamazi, Julai 15.
    Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholaus Musonye amesema katika Mkutano na Waandishi wa Habari mchana huu, ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ilala, Dar es Salaam kwamba, Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) itashiriki kama timu mualikwa.
    Aidha, habari za kusikitisha ni kwamba, Musonye amesema Sudan, Ethiopia, Eritrea na Somalia hazitaleta wawakilishi wao kwa sababu mbalimbali.
    Wakati Ethiopia ligi yao inaanza wiki hii, Sudan wawakilishi wao wapo kwenye michuano ya Afrika na wameshindwa kuteua timu mbadala, Somalia wawakilishi wao Elman wamebadilisha uongozi, hivyo bado hawajajipanga na Eritrea kutokana na desturi ya wachezaji wao kuzamia kila wanapokuja kwenye mashindano, wameondolewa.
    “Wameondolewa, kwa sababu mbili, kwanza nchi yao imeomba ipewe muda kulifanyia kazi sual hilo, na sisi pia (CECAFA) tunalitafutia ufumbuzi,”alisema Musonye.  
    Lakini Musonye amekiri kitendo cha kuyatoa mashindano hayo mwanzoni mwa mwaka hadi katikati ya mwaka kumechangia baadhi ya timu kutoshiriki na amesema tayari amewasilisha pendekezo kwenye Mkutano Mkuu, mashindano yarejee kufanyika mwanzoni mwa mwaka kama ilivyokuwa awali.
    Kuhusu mechi ya ufunguzi ya Simba kuchezwa Julai 16, ambayo itakuwa Jumatatu badala ya Jumapili, Musonye alisema kwamba imetokana na kwamba Julai 15, Uwanja wa Taifa kutakuwa na fainali za Copa Coca Cola, ambayo maandalizi yake yote yamekamilika.
    Yanga ndiye bingwa mtetezi wa mashindano, baada ya kuifunga Simba SC katika fainali mwaka jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.



    CECAFA CLUB KAGAME CUP 2012
    14th – 28th July 2012, Dar-Es Salaam, Tanzania
    Team Fixture list
     
    GROUP A             SIMBA(TZ), URA (UGA), VITA CLUB (CONGO DR) PORTS (DJB),
    GROUP B             AZAM(TZ), MAFUNZO(ZANZ), TUSKER (KEN),  
    GROUP C             YANGA(TZ), APR(RWD),WAU SALAAM (SOUTH SUDAN), ATLETICO(BUR),
     
    (QUALIFICATION: GROUP A 1st and 2nd AND 3rd GROUP B 1st and 2nd , GROUP C 1st and 2nd  AND 3rd QUALIFY TO QUARTER FINALS).
     
    DATE
    NO
    TEAMS
    GROUP
    VENUE
    TIME (EAT)
    Sat 14th July
    1
    2
    APR Vs WAU SALAAM
    YANGA v ATLETICO
    C
    C
    Dar
    Dar
    2pm
    4 PM
    Sun 15THJuly
    3
     
    AZAM V MAFUNZO
     
    B
     
    CHIMANZI
    4 PM
    Mon 16th July
    4
    5
    VITA CLUB Vs PORTS
    SIMBA Vs URA
    A
    A
    Dar
    Dar
    2PM
    4PM
    Tue 17th July
    6
    7
    ATLETICO Vs APR
    WAU SALAAM Vs YANGA
    C
    C
    Dar
    Dar
    2pm
    4PM
    Wed 18th July
    8
    9
    VITA CLUB Vs URA
    PORTS  Vs SIMBA
    A
    A
    Dar
    Dar
    2 pm
    4pm
    Thu 19th July
    10
    11
    ATLETICO Vs WAU Salam
    MAFUNZO Vs TUSKER
    C
    B
    Dar
    Dar
    2pm
    4pm
    Fri 20th July
    12
    13
    PORTS Vs URA
    YANGA Vs APR
    A
    C
    Dar
    Dar
    2pm
    4pm
    Sat 21st July
     
    14
    15
     
     
    AZAM Vs TUSKER
    SIMBA Vs VITA CLUB
     
     
    B
    A
     
     
    TBD
    TBD
    TBD
    TBD
     
    TBD
    Sun 22nd July
     
    REST DAY
     
     
     
     
     
    QUARTER FINALS
    Mon 23th July
    16
    17
    B2 Vs C2
    A1 Vs C3
     
     
    TBD
    TBD
    Tue 24th July
    18
    19
    C1 Vs A2
    B1 VsA3
     
    TBD
    TBD
    Wed 25th July
     
    REST DAY
     
     
    SEMI FINALS
    Thu 26th July
    20
    Winner 16 Vs Winner 17
     
    TBD
    TBD
    Thu 26th July
    21
    Winner 18 Vs Winner 19
     
    TBD
    TBD
     Fri 27th July
    REST DAY
    FINALS AND 3rd PLACE PLAY OFFS
    Sat 28th July
    22
    23
    Loser 20 Vs Loser 21
    Winner 20 Vs Winner 21
     
     
    TBD
    TBD
     

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA KUANZA NA URA, YANGA NA WARUNDI KAGAME, AZAM WAPEWA WAZENJI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top