• HABARI MPYA

    Sunday, January 29, 2017

    LWANDAMINA AWAANZISHA YONDAN, CANNAVARO, ZULU DHIDI YA MWADUI LEO

    Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
    KOCHA Mzambia George Lwandamina leo amewaanzisha pamoja wakongwe Kevin Yondan na Nadir Haroub 'Cannavaro' baada ya muda mrefu katika mchezo dhidi ya Mwadui FC.
    Pamoja na hao, Lwandamina amemuanzisha Mzambia mwenzake, Jutin Zulu katika safu ya kiungo upande wa ulinzi katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. 
    Nahodha wa Yanga, Nadir Cannavaro kulia akiwa na Justin Zulu kushoto, Wote wanaanza leo na Mwadui
    Vikosi vinavyoanza jioni ya leo Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam ni; Yanga SC; Deo Munishi 'Dida', Juma Abdul, Mwinyi Mngwali, Kevin Yondan, Nadir Haroub 'Cannavaro', Justin Zulu, Simon Msuva, Thabani Kamusoko, Amissi Tambwe, Haruna Niyonzima na Deus Kaseke.
    Mwadui FC; Shaaban Kado, Nassor Masoud 'Chollo', Malika Ndeule, Yassin Mustafa, Iddi Mobby, Razack Khalfan, Hassan Kabunda, Awadh Juma, Paul Nonga, Salim Khamis na Abdallah Seseme.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LWANDAMINA AWAANZISHA YONDAN, CANNAVARO, ZULU DHIDI YA MWADUI LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top