• HABARI MPYA

    Tuesday, January 24, 2017

    KITIMUTIMU CHAENDELEA KOMBE LA ASFC

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    MECHI za raundi ya tano ya mechi za Kombe la Shirikisho la Azam 2016/17 (Azam Sports Federation Cup - ASFC), zitaendelea kesho Jamatano Januari 25, 2017 kwa timu za Singida United na Kagera Sugar kucheza kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida.
    Mchezo mwingine utakaozikutanisha timu za The Mighty Elephant ya Songea na Mashujaa ya Kigoma katika mchezo utakaofanyika Uwanja Majimaji mjini Songea.
    Katika mchezo huo ambao uliahirishwa Jumatano iliyopita, mshindi wa kesho ndiye atacheza na Majimaji katika tarehe mpya itakayotangazwa hapo baadaye kama ilivyo kwa mechi kati ya African Lyon na Mshikamano.
    Leo Jumanne Januari 24, mwaka huu kuna mechi kati ya Mtibwa Sugar na Polisi Moro kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro wakati Kurugenzi ya Iringa itacheza na JKT Ruvu huko Mafinga huku Mbeya City ikipangwa kucheza na Kabela City Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya ilihali Madini na Panone zitacheza kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha. Pia Ndanda itacheza na Mlale JKT kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, mkoani Mtwara.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KITIMUTIMU CHAENDELEA KOMBE LA ASFC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top