IMEWEKWA SEPTEMBA 27, 2013 SAA 9:55 ALASIRI
Mshambuliaji wa Yanga SC, Mrisho Khalfan Ngassa (katikati) akiwa ameshika risiti ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya kulipa Sh. Milioni 45, alizotakiwa kuilipia klabu ya Simba SC. Wengine kulia ni Ofisa Habari wa Yanga SC, Baraka Kizuguto na kushoto Mhasibu, Rose Msamila. Ngassa alifungiwa mechi sita za mashindano na TFF pamoja na kutakiwa kurejesha fedha za Simba Sh. Milioni 30 na fidia ya Sh. Milioni 15, baada ya kubainika alisaini timu mbili, Simba na Yanga alikoidhinishwa kuchezea msimu huu.
|