IMEWEKWA SEPTEMBA 19, 2013 SAA 6:53 USIKU
ARSENAL imeanza vyema Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kushinda ugenini mabao 2-1 dhidi ya wenyeji, Marseille Uwanja wa Velodrome, Ufaransa.
Mabao ya Gunners yalifungwa na Theo Walcott dakika ya 65 na Aaron Ramsey dakika ya 83, wakati la wenyeji lilifungwa na Jordan Ayew kwa penalti dakika ya 90.
Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Szczesny, Gibbs, Koscienly, Mertesacker, Sagna, Flamini/Myaichi dk90, Wilshere, Ramsey, Ozil, Walcott/Monreal dk77 na Giroud.
Marseille: Mandanda, Fanni, N'Koulou, Mendes, Morel, Romao, Imbula/Thauvin dk79, Payet/J.Ayew dk72, Valbuena/Khalifa dk89, A. Ayew na Gignac.

Kitu hicho: Theo Walcott ameifungia Arsenal


Kitu kingine: Aaron Ramsey amefunga bao la sita msimu huu


Si mchezo wangu: Mesut Ozil alicheza kiungwana katika ukabaji wake

Kipaji: Theo Walcott akipambana na kiungo wa Marseille, Mathieu Valbuena

Yuko juu: Jack Wilshere alicheza vizuri katika nafasi ya kiungo

Sito rafu? Buti la juu likimuelekea Mathieu Flamini

Rekodi ya klabu: Arsenal imetweet mechi zake 10 ilizoshinda ugenini

Hafunguki kwa urahisi: Steve Mandanda aliibania Arsenal hadi dakika ya 65

Yalaaa: Arsenal walifikiri walistahili kupewa penalti baada ya buti hili alilopigwa Per Mertesacker

Yuko juu: The Gunners ina sababu za kujivunia Ozil

La kufuta machozi: Jordan Ayew akifunga kwa penalti

Mchapakazi: Flamini alionyesha yeye ni mchezaji hodari


Mgumu: Arsene Wenger (kulia) atafurahia Mertesacker na Wojciech Szczesny (kushoto) wasiporuhusu mabao

Nambari moja: Walcott akiupungua umati wa mashabiki baada ya mechi

Alipigana: Olivier Giroud alishindwa, kufunga licha ya kupambana


.png)