IMEWEKWA AGOSTI 15, 2013 SAA 1:12 ASUBUHI
ENGLAND jana imewafunga wapinzani wao, Scotland, mabao 3-2 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Wembley.
Mabao ya England yalifungwa na Theo Walcott dakika ya 29, Danny Welbeck dakika ya 53 na RickieLambert dakika ya 70, Scotland ilitangulia kupata mabao yake kupitia kwa Morrison dakika ya 11 na Miller 49.
Kikosi cha England kilikuwa Hart, Walker, Cahill, Jagielka/Jones dk84, Baines, Cleverley/Milner dk67, Gerrard/Oxlade-Chamberlain dk62, Wilshere/Lampard dk46, Walcott/Zaha dk75 na Rooney.
Scotland: McGregor, Hutton, Martin, Hanley, Whittaker, Snodgrass/Conway dk66, Morrison/Rhodes dk82, Brown, Forrest/Mulgrew dk67, Maloney/Naismith dk86, Miller/Griffiths dk73.

Rickie Lambert akiifungia bao la ushindi England

Lambert akishangilia na Frank Lampard baada ya kufunga


Rooney akipambana na alisababisha bao la ushindi lililofungwa na Lambert

Rooney akigeuka kutoka upande wa mashabiki wa Scotland

James Morrison akifumua shuti kumtungua Joe Hart

Shuti la Morrison likielekea moja kwa moja nyavuni

Kitu nyavuni

Majanga:... na Hart anashuhudia nyavu zake zinatikisika

Unaikumbuka hii? Mchezaji wa zamani wa Scotland, Gordon McQueen akiifungia nchi yake katika Uwanja huo huo mwaka 1977

Theo Walcott akielekea kufunga akiwa ndani ya eneo la penalti

Baada ya kumtoka beki, Walcott alifumua shuti hadi nyavuni

Bonge la bao...mambo ya Walcott

Asante Theo! Tom Cleverley akimkumbatia winga wa Arsenal baada ya kufunga

Kenny Miller akiifungia Scotland

Gary Cahill...

Miller akishangilia baada ya kuwapa wapinzani wa England bao la kuongoza

La kusawazisha: Danny Welbeck aliisawazishia England

Welbeck amefunga bao la sita tangu aanze kuichezea England

Wachezaji wa England akiwemo Wayne Rooney (katikati) wakishangilia bao la kusawazisha la Welbeck

Rooney akiondoka kinyonge uwanjani.
KWA MATOKEO YA MECHI NYINGINE ZOTE ZA KIRAFIKI JANA, SHUKA CHINI KABISA YA UKURASA
KWA MATOKEO YA MECHI NYINGINE ZOTE ZA KIRAFIKI JANA, SHUKA CHINI KABISA YA UKURASA


.png)