• HABARI MPYA

    Sunday, August 11, 2013

    CHELSEA YAILAZA 2-1 ROMA, LUKAKU AZIDI KUMPA RAHA MOURINHO

    IMEWEKWA AGOSTI 11, 2013 SAA 1:11 USIKU
    MABAO ya Romelu Lukaku na kiungo mkongwe, Frank Lampard yameipa Chelsea ushindi wa 2-1 dhidi ya AS Roma katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na msimu mjini Washington.
    Kiungo huyo alifunga bao kwa shuti la mbali ambalo lilikuwa la kusawazisha dakika ya 60, baada ya Eric Lamela kutangulia kuifungia Roma dakika ya 20.
    Romelu Lukaku akaendelea kumpa raha kocha Jose Mourinho, baada ya kufunga bao la dakika ya 89.
    Katika mchezo wa huo, kikosi cha Chelsea kilikuwa: Schwarzer/Blackman dk46, Azpilicueta/Ivanovic dk57, Luiz/Cahill dk46, Terry/Lukaku dk78, Bertrand, Mikel/Van Ginkel dk57, Essien/Lampard dk46, Moses/Ramires dk46, De Bruyne/Oscar dk46, Schurrle/Hazard dk57 na Torres/Ba dk46.
    Roma: De Sanctis; Maicon/Jedvaj dk78, Benatia, Castan, Balzaretti; Bradley, Strootman, Florenzi/Marquinho dk69, Lamela, Osvaldo/Borriello dk69 na Totti/Tallo dk85.
    Helping hand: Chelsea midfielder Frank Lampard celebrates his goal against Roma with his team-mates
    Kiungo wa Chelsea, Frank Lampard akishangilia na wachezaji wenzake baada ya kufunga
    Blunder: Roma's Erik Lamela opened the scoring, taking advantage of a mistake from Mark Schwarzer
    Mchezaji wa Roma, Erik Lamela akiifungia timu yake bao la kuongoza kufuatia makosa ya kipa Mark Schwarzer
    All smiles: Chelsea head coach Jose Mourinho shakes hands with Roma goalkeeper Morgan de Sanctis
    Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho akisalimiana na kipa wa Roma, Morgan de Sanctis
    Tough tackling: Roma defender Mehdi Benatia (left) fights for the ball against Chelsea midfielder Eden Hazard
    Beki wa Roma, Mehdi Benatia (kushoto) akipambana na kiungo wa Chelsea, Eden Hazard
    Winner: Morgan de Sanctis turns to watch as Chelsea's Romelu Lukaku scores late on
    La ushindi: Morgan de Sanctis akishuhudia mpira uliopigwa na mshambuliaji wa Chelsea, Romelu Lukaku ukitinga nyavuni
    Chelsea's Romelu Lukaku (L) celebrates his goal
    Lukaku akishangilia na wenzake baada ya kufunga bao la ushindi

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: CHELSEA YAILAZA 2-1 ROMA, LUKAKU AZIDI KUMPA RAHA MOURINHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top