• HABARI MPYA

    Thursday, November 29, 2012

    ZANZIBAR KUJARIBU BAHATI TENA LEO TUSKER CHALLENGE, KUKIPIGA NA RWANDA NI VITA YA NIYONZIMA NA CANNAVARO

    Zanzibar Heroes

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    MASHUJAA wa visiwani, Zanzibar Heroes leo wanatupa kete yao ya pili katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge kwa kumenyana na Rwanda katika mchezo wa Kundi C, utakaoanza saa 12:00 jioni Uwanja wa Mandela, Namboole, mjini hapa.
    Mchezo huo utatanguliwa na mchezo mwingine, kati ya Malawi na Eritrea ambao utaanza saa 10:00 jioni kwenye Uwanja huo.
    Zanzibar walilazimishwa sare ya bila kufungana na Eritrea katika mchezo wa kwanza, wakati Malawi ilifungwa mabao 2-0 na Rwanda.
    Zanzibar wanahitaji kushinda mechi ya leo, ili kuweka hai matumaini ya kuingia Robo Fainali ya michuano hii, ingawa mbele ya Rwanda huo utakuwa mtihani mgumu kwao.
    Moja kati ya burudani zinazotarajiwa kwenye mechi hiyo ni kushuhudia wachezaji wawili wa klabu moja, Yanga SC ya Dar es Salaam, beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ wa Zanzibar na kiungo Haruna Niyonzima wa Rwanda, wakichuana leo, tena wote wakiwa manahodha wa timu zao za taifa.
    Baada ya sare katika mechi ya kwanza, Cannavaro pamoja na kuwaomba radhi Wazanzibari kwa sare hiyo, lakini pia ameahidi watajituma na kufanya vizuri katika mechi zijazo. 

    MECHI ZILIZOSALIA:
    RATIB KUNDI A:
    Novemba 30, 2012:
    Kenya v Ethiopia                  (Saa 9:00 Alasiri)
    Sudan Kusini v Uganda       (Saa 12:00 jioni)
    RATIBA KUNDI B:
    Desemba 1, 2012:
    Sudan v Burundi                 (Saa 9:00 Alasiri)
    Somalia v Tanzania             (Saa 12:00 jioni)
    RATIBA KUNDI C:
    Novemba 29, 2012:
    Malawi v Eritrea                   (Saa 9:00 Alasiri)
    Rwanda v Zanzibar             (Saa 12:00 jioni)
    Desemba 2, 2012:
    Malawi v Zanzibar               (Saa 9:00 Alasiri)
    Eritrea v Rwanda                (Saa 12:00 jioni)

    MSIMAMO KUNDI A:
                          P   W  D   L    GF GA GD Pts
    Uganda          2    2    0    0    2    0    2    6
    Kenya             2    1    0    1    2    1    1    3
    Ethiopia          2    1    0    1    1    1    0    3
    Sudan Kusini  2    0    0    2    0    3    -3  0

    MSIMAMO KUNDI B:
                         P   W  D   L    GF GA GD Pts
    Burundi         2    2    0    0    6    1    5    6
    Tanzania       2    1    0    1    2    1    1    3
    Sudan           2    1    0    1    1    2    -1  3
    Somalia         2    0    0    2    1    6    -5  0

    MSIMAMO KUNDI C:
                          P   W  D   L    GF GA GD Pts
    Rwanda         1    1    0    0    2    0    2    3
    Eritrea            1    0    1    0    0    0    0    1
    Zanzibar         1    0    1    0    0    0    0    1
    Malawi            1    0    0    1    0    2    -2  0

    VIWANGO VYA UBORA FIFA
    NCHI                 NAFASI
    Uganda             86
    Malawi              101
    Ethiopia            102
    Sudan               102
    Rwanda             122
    Burundi             128
    Kenya                130
    Tanzania           134
    Zanzibar            134
    Somalia             193
    Eritrea               192
    Sudan Kusini     200
    (Viwango hivi vimetoka mwezi huu)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ZANZIBAR KUJARIBU BAHATI TENA LEO TUSKER CHALLENGE, KUKIPIGA NA RWANDA NI VITA YA NIYONZIMA NA CANNAVARO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top