• HABARI MPYA

    Thursday, November 29, 2012

    MALAWI YAWAFUNGA KWA MBINDE ERITREA

    Mshambuliaji wa Malawi, Rodrick Gonani akimtoka beki wa Eritrea, Yohannes Nega katika mchezo wa Kundi C, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge, uliofanyika kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala, Uganda jioni hii. Malawi ilishinda 3-2, mabao ya Chiukepo Msowoya dakika ya nne, Miciam Mhone dakika ya 10 na Patrick Masanjala dakika ya 66, wakati ya Eritrea yalifungwa na Amir Hamad Omary dakika ya 72 na Yosief Ghide kwa penalti dakika ya 89. 

    Kocha wa Rwanda, Milutin Sredojevic ‘Micho’ akiwa na wasaidizi wake, Mugisha Ibrahim ambaye ni kocha wa makipa na Eric Nshimiyimana, ambaye ni Kocha Msaidizi, wakifuatilia mchezo wa Kundi C kati ya Malawi na Eritrea Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala, Uganda.

    Kocha wa Tanzania, Kim Poulsen akiwa na Msaidizi wake, Sylvester Marsh wakifuatilia mchezo kati ya Rwanda na Malawi. Chini ni Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MALAWI YAWAFUNGA KWA MBINDE ERITREA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top