Mshambuliaji wa timu ya Tanzania Bara, Kilimanjaro
Stars, John Bocco wa Azam FC ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, akiwangoza wenzake kutoka Uwanja wa Ndege wa Entebe, Uganda jana kwa ajili ya michuano ya Kombe la Mataifa
ya Afrika Mashariki na Kati, Tusker Challenge inayoanza leo mjini hapa Kampala,
Uganda. Stars imefikia hoteli ya Mt Zion na itakuwa ikifanya mazoezi Nakawa,
wakati kesho itaanza kampeni zake kwa kumenyana na Sudan, Uwanja wa Mandela, Namboole
sa 12:00 jioni. |