• HABARI MPYA

    Friday, November 30, 2012

    JOHN BOCCO AGEUKA LULU KUJMPALA, WATU WAANZA KUFIKA BEI

    John Bocco

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    SOKA ya nguvu aliyoonyesha mshambuliaji wa Tanzania Bara, John Bocco ‘Adebayor’ katika mechi mbili za Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge zimemfanya awe lulu katika mashindano haya yanayoendelea mjini hapa.
    Mawakala mbalimbali waliopo mjini Kampala wameanza kuulizia uwezekano wa kumtafutia timu Ulaya mchezaji huyo wa Azam, lakini uongozi wa timu ya Bara, Kilimanjaro Stars mjini hapa umewataka wawasiliane na klabu yake, Azam FC ya Dar es Salaam moja kwa moja.
    Lakini pia kuna uwezekano klabu ya SuperSport United ya Afrika Kusini, iliyomfanyia majaribio Agosti mwaka huu ikamfikiria tena mchezaji huyo kutokana na kiwango kikubwa alichoonyesha hadi sasa kwenye mashindano haya.
    Japokuwa hakufunga bao juzi kwenye mechi na Burundi, lakini kazi aliyoifanya wengi walikubali yeye ni mshambuliaji mzuri haswa kutokana na mfumo wa sasa wa kocha wa Stars, Mdenmark Kim Poulsen kumtumia peke yake mbele.  
    Bocco ana mabao mawili kwa sasa, wakati mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Suleiman Yamin Ndikumana ndiye anayeongoza kwa mabao katika michuano hii.
    Ndikumana aliyewahi pia kucheza Norway na Uturuki, juzi alifunga bao la tatu katika mashindano haya, akiichezea Burundi dhidi ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars. 
    Jumla ya mabao 25 hadi sasa yamefungwa katika mechi 18 za makundi yote matatu, zilizopigwa kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala.
    Bocco anafungana na mshambuliaji mwingine wa Burundi, Christopher Nduwarugira na mchezaji mwenzake wa Azam, Khamis Mcha ‘Vialli’ wakati wachezaji wengine ambao hadi sasa kila mmoja amefunga bao moja ni Farid Mohamed, Yussuf Ndikumana wa Burundi, Mohamed Jabril wa Somalia kwa penalti, Geoffrey Kizito wa Uganda, Yonatal Kebede Teklemariam, Haruna NiyonzimUganda, David Ochieng, Clifton Miheso na Jean Mugiraneza, Dadi Birori, Chiukepo Msowoya, Miciam Mhone, Patrick Masanjala, Amir Hamad Omary na Yosief Ghide.

    WAFUNGAJI CECAFA TUSKER CHALLENGE 2012
    Suleiman Ndikumana    Burundi    3 (1 penalti)
    John Bocco                   Tanzania  2
    Khamis Mcha                Zanzibar   2
    Chris Nduwarugira        Burundi    2 
    Yussuf Ndikumana        Burundi    1
    Mohamed Jabril            Somalia    1(penalti).
    Geoffrey Kizito              Uganda    1
    Brian Umony                 Uganda    1
    Yonatal Teklemariam    Ethiopia    1
    Haruna Niyonzima        Rwanda    1
    Jean Mugiraneza          Rwanda    1
    Dadi Birori                    Rwanda    1
    David Ochieng             Kenya       1
    Clifton Miheso              Kenya       1
    Farid Mohamed            Sudan      1
    Chiukepo Msowoya      Malawi      1
    Miciam Mhone              Malawi      1
    Patrick Masanjala         Malawi      1
    Amir Hamad Omary      Eritrea      1
    Yosief Ghide                Eritrea       1(penalti)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: JOHN BOCCO AGEUKA LULU KUJMPALA, WATU WAANZA KUFIKA BEI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top