• HABARI MPYA

    Monday, November 26, 2012

    ZANZIBAR HEROES WAANZA KAZI LEO KAMPALA

    Zanzibar Heroes watang'ara leo?

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    TIMU ya soka ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes leo inaanza kampeni zake za kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge kwa kumenyana na Eritrea katika mchezo wa Kundi C, utakaonza saa 9:00 alasiri Uwanja wa Mandela, Namboole mjini hapa
    Mchezo huo, utafuatiwa na mchezo mwingine wa kundi hilo, ambao unatarajiwa kuwa mkali zaidi na wa kusisimua kati ya Rwanda na Malawi kuanzia saa saa 12:00 jioni.
    Kikosi cha Zanzibar Heroes kiliagwa Jumatano visiwani Zanzibar katika Hoteli ya Bwawani ambayo inamilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo, Said Ali Mbarouk.
    Kikosi kiliondoka Alhamisi Zanzibar kuaa Kampala kikipitia Dares Salaam na kimeondoka na msafara wa watu 30, wakiwemo wachezaji 20, benchi la ufundi na viongozi wa Serikali na Chama cha Soka Visiwani Zanzibar (ZFA).
    Hata hivyo, Heroes itamkosa kiungo wake mahiri Abdulhalim Humud, ambaye ni majeruhi.
    Kikosi kinachotarajiwa kuanza leo Heroes ni; Mwadin Ali Mwadini, Nassor Masoud ‘Cholo’, Samir Hajji Nuhu, Agrey Moris, Nadir Haroub Ali 'Canavaro, Sabri Ali, Khamis Mcha 'Vialli', Is-haka Othman, Amir Hamad, Twaha Mohammed na Suleiman Kassim ‘Selembe’.
    Tayari mechi za awali za Kundi A na B zimekwishachezwa na leo Kundi C ndio linafichua makali yake kwa mara ya kwanza.
    Katika mechi za ufunguzi za Kundi A, Ethiopia waliifunga Sudan Kusini 1-0, wakati Uganda waliichapa Kenya 1-0 pia juzi, Uwanja wa Mandela, Namboole.
    Mechi za Kundi B jana, Burundi iliitandika Somalia mabao 5-1, kabla ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars kuilaza Sudan 2-0.   
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ZANZIBAR HEROES WAANZA KAZI LEO KAMPALA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top