• HABARI MPYA

    Thursday, November 29, 2012

    NDIKUMANA AWATEGA SIMBA SC

    Ndikumana

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    MSHAMBULIAJI wa zamani wa Simba SC, Suleiman Yamin Ndikumana kwa sasa ndiye anaongoza kwa kufunga mabao katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge inayoendelea mjini hapa.
    Ndikumana aliyewahi pia kucheza Norway na Uturuki, jana alifunga bao la tatu katika mashindano haya, akiichezea Burundi dhidi ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars. 
    Sasa anamzidi kwa bao moja, John Bocco ‘Adebayor’ wa Kilimanjafo Stars.
    Jumla ya mabao 17 hadi sasa yamefungwa katika mechi 16 za makundi yote matatu, zilizopigwa kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala.
    Bocco anafungana na mshambuliaji mwingine wa Burundi, Christopher Nduwarugira, wakati wachezaji wengine ambao hadi sasa kila mmoja amefunga bao moja ni Farid Mohamed, Yussuf Ndikumana wa Burundi, Mohamed Jabril wa Somalia kwa penalti, Geoffrey Kizito wa Uganda, Yonatal Kebede Teklemariam, Haruna NiyonzimUganda, David Ochieng, Clifton Miheso na Jean Mugiraneza.
    Kwa sasa Bocco anayechezea Azam FC ya Dar es Salaam, ndiye mshambuliaji pekee kwenye kikosi cha Bara, baada ya washambuliaji wengine, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaochezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemomkrasia ya Kongo (DRC) kuzuiliwa na klabu yao.

    WAFUNGAJI CECAFA TUSKER CHALLENGE 2012
    Suleiman Ndikumana   Burundi    3 (1 penalti)
    John Bocco                  Tanzania  2
    Chris Nduwarugira        Burundi   2
    Yussuf Ndikumana       Burundi   1
    Mohamed Jabril            Somalia   1(penalti).
    Geoffrey Kizito              Uganda   1
    Brian Umony                 Uganda   1
    Yonatal Teklemariam     Ethiopia  1
    Haruna Niyonzima         Rwanda  1
    Jean Mugiraneza           Rwanda  1
    David Ochieng               Kenya     1
    Clifton Miheso                Kenya     1
    Farid Mohamed              Sudan     1 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: NDIKUMANA AWATEGA SIMBA SC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top