• HABARI MPYA

    Saturday, November 24, 2012

    KIPYENGA CHA KWANZA TUSKER CHALLENGE 2012 LEO

    Uganda, mabingwa watetezi wanaanza na Kenya leo. Patachimbika Namboole

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    MICHUANO ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, Tusker Challenge inatarajiwa kuanza kutimua vumbi leo kwenye Uwanja wa Mandela, uliopo Namboole, mjini Kampala, Uganda.
    Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Mcameroon, Issa Hayatou tayari yupo mjini hapa kwa ajili ya kufungua michuano hiyo na jana alihudhuria Mkutano Mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) katika hoteli ya Serena.
    Wenyeji na mabingwa watetezi, Uganda ‘The Cranes’ watashuka dimbani saa 12:00 jioni kupepetana na jirani zao, Kenya ‘Harambee Stars’ katika mchezo mkali na wa kusisimua, kulingana na historia ya timu hizo zinapokutana.
    Mchezo huo, utatanguliwa na mechi kati ya majirani wengine, Sudan Kusini na Ethiopia itakayoanza saa Saa 9:00 Alasiri, ambayo nayo pia inatarajiwa kuwa kali nay a kusisimua.
    Mechi hizi za Kundi A, ambalo linastahili kuitwa Kundi la kifo, zitafuatiwa na mechi za Kundi B kesho, kati ya Burundi na Somalia Saa 9:00 Alasiri na baadaye, saa 12 jioni Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ watakuwa na kibarua kizito mbele ya Sudan.
    Bara ambayo inajivunia kutwaa mara tatu Kombe la Challenge katika miaka ya 1974, 1994 na 2010, iliwasili hapa jana jioni na kufikia katika hoteli ya Mt Zion, ambako pia wamefikia Ethiopia, wawakilishi wa CECAFA katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika Januari mwakani nchini Afrika Kusini.
    Stars iliyopangiwa kufanya mazoezi katika Uwanja wa Nakawa, itarudi tena dimbani, Novemba 28 kukipiga na Burundi, mchezo utakaotanguliwa na mechi kati ya Somalia na Sudan kabla ya kuhitimisha mechi zake za kundi hilo kwa kumenyana na Somalia Desemba 1, mchezo utakaotanguliwa na mechi nyingine kati ya Sudan na Burundi.
    Michuano hii, imedhaminiwa na Kampuni ya Bia Afrika Mashariki (EABL), kupitia bia yake ya Tusker Lager, kwa dau lao la dola za Kimarekani 450,000.
    Udhamini wa mwaka huu huo ni ongezeko la aslimia 5, kutoka michuano ya mwaka jana mjini Dar es Salaam, ambayo Uganda waliibuka mabingwa.
    Ni udhamini ambao utahusu usafiri, malazi na huduma nyingine, wakati jumla ya dola za Kimarekani 60.000 zitakuwa kwa ajili ya zawadi, bingwa akipewa dola 30.000, mshindi wa pili dola 20.000 na dola 10.000 mshindi wa tatu.   Kama ilivyo ada, mechi zote za michuano hiyo zitaonyeshwa na Televisheni ya Super Sport ya Afrika Kusini.

    MAKUNDI RATIBA TUSKER CHALLENGE 2012:
    KUNDI A: Uganda, Kenya, Ethiopia na Sudan Kusini
    KUNDI B: Tanzania, Sudan, Burundi na Somalia
    KUNDI C: Malawi, Eritrea, Rwanda na Zanzibar

    RATIB KUNDI A:
    Novemba 24, 2012:
    Ethiopia v Sudan                   (Saa 9:00 Alasiri)
    Uganda v Kenya                    (Saa 12:00 jioni)
    Novemba 27, 2012:
    Sudan Kusini v Kenya           (Saa 9:00 Alasiri)
    Uganda v Ethiopia          (Saa 12:00 jioni)
    Novemba 30, 2012:
    Kenya v Ethiopia                   (Saa 9:00 Alasiri)
    Sudan Kusini v Uganda (Saa 12:00 jioni)

    RATIBA KUNDI B:
    Novemba 25, 2012:
    Burundi v Somalia          (Saa 9:00 Alasiri)
    Tanzania v Sudan                 (Saa 12:00 jioni)
    Novemba 28, 2012:
    Somalia v Sudan                   (Saa 9:00 Alasiri)
    Tanzania v Burundi        (Saa 12:00 jioni)
    Desemba 1, 2012:
    Sudan v Burundi             (Saa 9:00 Alasiri)
    Somalia v Tanzania        (Saa 12:00 jioni)

    RATIBA KUNDI C:
    Novemba 26, 2012:
    Zanzibar v Eritrea           (Saa 9:00 Alasiri)
    Rwanda v Malawi           (Saa 12:00 jioni)
    Novemba 29, 2012:
    Malawi v Eritrea                   (Saa 9:00 Alasiri)
    Rwanda v Zanzibar         (Saa 12:00 jioni)
    Desemba 1, 2012:
    Malawi v Zanzibar          (Saa 9:00 Alasiri)
    Eritrea v Rwanda                  (Saa 12:00 jioni)

    ROBO FAINALI:
    Desemba 3, 2012
    Mshindi Kundi C vs Mshindi wa Pili Kundi B (Saa 10:00 jioni)
    Mshindi Kundi A vs Mshindi wa Tatu Bora wa pili (Saa 1:00 usiku)
    Desemba 4, 2012 (16:00):
    Mshindi Kundi B vs Mshindi wa Tatu Bora wa kwanza (Saa 10:00 jioni)
    Mshindi wa Pili Kundi A vs Mshindi wa Pili Kundi C       (Saa 1:00 usiku)

    NUSU FAINALI:
    Desemba 6, 2012
    Nusu Fainali ya Kwanza       (Saa 10:00 jioni)
    Nusu Fainali ya Pili         (Saa 1:00 usiku)

    MSHINDI WA TATU:
    Desemba 8, 2012
    Waliofungwa Nusu Fanali (Saa 10:00 jioni)

    FAINALI:
    Desemba 8, 2012
    Walioshinda Nusu Fainali  (Saa 1:00 usiku)

    ORODHA YA MABINGWA CHALLENGE;
    Mwaka Bingwa         
    1973     Uganda     
    1974     Tanzania   
    1975     Kenya      
    1976     Uganda     
    1977     Uganda     
    1978     Malawi     
    1979     Malawi     
    1980     Sudan      
    1981     Kenya      
    1982     Kenya      
    1983     Kenya      
    1984     Zambia     
    1985     Zimbabwe   
    1986     Haikufanyika
    1987     Ethiopia   
    1988     Malawi     
    1989     Uganda     
    1990     Uganda     
    1991     Zambia     
    1992     Uganda     
    1993     Haikufanyika
    1994     Tanzania   
    1995     Zanzibar   
    1996     Uganda     
    1997     Haikufanyika
    1998     Haikufanyika    
    1999     Rwanda B   
    2000     Uganda     
    2001     Ethiopia   
    2002     Kenya      
    2003     Uganda     
    2004     Ethiopia   
    2005     Ethiopia   
    2006     Zambia     
    2007     Sudan      
    2009     Uganda     
    2009     Uganda 
    2010     Tanzania Bara
    2011     Uganda
    2012     ?????

    VIWANGO VYA UBORA FIFA
    NCHI                 NAFASI
    Uganda             86
    Malawi              101
    Ethiopia            102
    Sudan               102
    Rwanda             122
    Burundi             128
    Kenya                130
    Tanzania           134
    Zanzibar            134
    Somalia             193
    Eritrea               192
    Sudan Kusini     200
    (Viwango hivi vimetoka mwezi huu)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: KIPYENGA CHA KWANZA TUSKER CHALLENGE 2012 LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top