Kiungo wa
Kenya, Kevin Omondi akimdhibiti mshambuliaji wa Sudan Kusini, Martin Kamis
anayejaribu kuondoka na mpira katika mechi ya Kundi A, Kombe la Mataifa ya
Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge, Uwanja wa Mandela, Namboole,
Kampala, Uganda jioni hii. Kenya ilishinda 2-0 mabao ya David Ochieng dakika ya
24 na Clifton Miheso dakika ya 72. Kenya sasa inaongoza Kundi A kwa wastani wa
mabao, ikiwa na pointi sawa na Uganda na Ethiopia ambazo zinamenyana baadaye
kidogo.
|