• HABARI MPYA

    Monday, November 26, 2012

    BOCCO ANAVYOTISHA KAMPALA, BADO WASOMALI NA WARUNDI WATAMKOMA

    John Raphael Bocco 'Adebayor', atatwaa kiatu cha dhahabu CECAFA Tusker Challenge 2012?

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    JOHN Bocco ‘Adebayor’ ameingia kwenye orodha ya wachezaji wanaowania ufungaji bora wa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge kufuatia jana kufunga mabao mawili, Tanzania Bara ikiilaza Sudan 2-0 katika mchezo wa Kundi B, Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala, Uganda.
    Bocco aliyeifungia Kilimanjaro Stars, inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager mabao yote hayo kipindi cha kwanza, sasa analingana na washambuliaji wa Burundi, Chris Nduwarugira na Suleiman Ndikumana, ambao kila mmoja ana mabao mawili pia.
    Wengine ambao hadi sasa kila mmoja amefunga bao moja ni Yussuf Ndikumana wa Burundi, Mohamed Jabril wa Somalia kwa penalti, Geoffrey Kizito wa Uganda na Yonatal Kebede Teklemariam.
    Bocco ana nafasi zaidi ya kuongeza mabao katika mechi za kundi hilo, haswa kwenye mchezo dhidi ya Somalia Desemba 1, kwani hiyo ndio timu dhaifu zaidi kwenye Kundi B.
    Lakini Bocco kama atacheza kwa kiwango cha jana, anaweza akawa mwiba hata mbele ya Burundi Novemba 28.
    Kwa sasa Bocco anayechezea Azam FC ya Dar es Salaam, ndiye mshambuliaji pekee kwenye kikosi cha Bara, baada ya washambuliaji wengine, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaochezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemomkrasia ya Kongo (DRC) kuzuiliwa na klabu yao.

    WAFUNGAJI CECAFA TUSKER CHALLENGE 2012
    John Bocco                  Tanzania 2
    Yussuf Ndikumana       Burundi   2
    Suleiman Ndikumana   Burundi   2
    Yussuf Ndikumana       Burundi   1
    Mohamed Jabril            Somalia   1(penalti).
    Geoffrey Kizito              Uganda    1
    Yonatal Teklemariam    Ethiopia   1 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: BOCCO ANAVYOTISHA KAMPALA, BADO WASOMALI NA WARUNDI WATAMKOMA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top