• HABARI MPYA

    Thursday, July 18, 2019

    TAIFA STARS YAPANGWA NA TUNISIA, LIBYA NA EQUATORIAL GUINEA KUFUZU AFCON 2021

    Na Mwandishi Wetu, CAIRO
    TANZANIA imepangwa Kundi J kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika 2021 nchini Cameroon pamoja na Tunisia, Libya na Equatorial Guinea.
    Tunisia ilifungwa na Nigeria 1-0 jana katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu AFCON 2019 nchini Misri na Tanzania ilifungwa mechi zote tatu za Kundi C 2-0 na Senegal, 3-2 na Kenya na 3-0 na Algeria.
    Libya na Equatorial Guinea zote hazikufuzu fainali za AFCON mwaka huu ambazo zimeshuhudia timu za Kundi C tupu, Algeria na Senegal zikiingia fainali.
    Kenya iliyokuwa kundi moja na Tanzania kwenye fainali za mwaka huu, yenyewe kwenye mbio za Cameroon 2021 imepangwa Kundi G na Misri, Togo na Comoro na mechi za kwanza zitachezwa kati ya Novemba 7 na 11.
    Uganda wamepangwa Kundi B pamoja na Burkina Faso, Malawi na ama Sudan Kusini au Shelisheli, wakati Algeria imepangwa Kundi H pamoja na Zambia, Zimbabwe na Botswana na Senegal ipo Kundi I pamoja na Kongo, Guinea Bissau na Eswatini.

    MAKUNDI YOTE KUFUZU AFCON 2021 CAMEROON
    Kundi A: Mali, Guinea, Namibia, Liberia/Chad
    Kundi B: Burkina Faso, Uganda, Malawi, Sudan Kusini/Shelisheli
    Kundi C: Ghana, Afrika Kusini, Sudan, Mauritius/Sao Tome
    Kundi D: DRC, Gabon, Angola, Djibouti v Gambia
    Kundi E: Morocco, Mauritania, CAR, Burundi
    Kundi F: Cameroon, Cape Verde, Msumbiji, Rwanda
    Kundi G: Misri, Kenya, Togo, Comoro
    Kundi H: Algeria, Zambia, Zimbabwe, Botswana
    Kundi I: Senegal, Congo, Guinea Bissau, Eswatini
    Kundi J: Tunisia, Libya, Tanzania, Equatorial Guinea
    Kundi K: Ivory Coast, Niger, Madagascar, Ethiopia
    Kundi L: Nigeria, Benin, Sierra Leone, Lesotho
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS YAPANGWA NA TUNISIA, LIBYA NA EQUATORIAL GUINEA KUFUZU AFCON 2021 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top