BONDIA Tyson Fury anatarajiwa kupanda ulingoni Oktoba 24, mwaka huu kuzipiga na Wladimir Klitschko nchini Ujerumani katika pambano la ubingwa wa dunia uzito wa juu.
Makubaliano ya pambano hilo yamefikiwa leo na wababe hao wanatarajiwa kwenda kuzichapa mjini Dusseldorf.
Fury ametweet juu ya Klitschko leo: "Haijalishi pambano hili litafanyika wapi, Ukraine, Deutschland, Japan, itakuwa yale yale kumtwanga tu,".
0 comments:
Post a Comment