MKONGWE Andrea Pirlo ameondoka rasmi Juventus kuhamia New York City, klabu zote zimethibitisha.
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Italia amecheza kwa miaka minne Juve ikiwa Serie A, na sasa ataungana na kiungo mwenzake mkongwe wa England, Frank Lampard timu hiyo ya Ligi Kuu Marekani, maarufu kama Major League Soccer itakayoanza Julai 21.
Pirlo anayetarajiwa kusaini Mkataba wa miezi 18, ameiambia tovuti ya klabu hiyo: "Nimekuwa nikihitaji uzoefu huu kwa muda mrefu na sasa fursa hii imekuja nataka kuichukua,"amesema.
Pirlo sasa ataungana na mkongwe mwenzake Frank Lampard kuanzia Julai 21 Ligi Kuu ya Marekani PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment