• HABARI MPYA

    Sunday, July 26, 2015

    MECHI YA YANGA NA AZAM FC YANUKIA ROBO FAINALI KAGAME 2015, ITAKUWA JUMATANO

    Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
    MECHI ya mahasimu wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Azam FC na Yanga SC inanukia katika Robo Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki, Kombe la Kagame mapema wiki ijayo.
    Yanga SC leo wanacheza mechi yao ya mwisho ya Kundi A Kombe la Kagame dhidi ya Khartoum N ya Sudan Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia Saa 10:00 jioni.
    Mchezo huo utatanguliwa na mechi nyingine ya kundi hilo kati ya Gor Mahia ya Kenya na Telecom ya Djibouti.
    KMKM ya Zanzibar imemaliza mechi zake za kundi hilo na imekwisharejea Zanzibar baada ya kutolewa kufuatia kuambulia pointi tatu za ushindi wa mechi moja dhidi ya vibonde, Telecom 1-0.

    Mshambuliaji wa Yanga SC, Kpah Sherman (kushoto) akiwania mpira dhidi ya beki wa Azam FC, Shomary Kapombe katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu. Je, timu hizo zitakutana Robo Fainali Kombe la Kagame?

    Telecom wamefungwa na kila timu katika kundi hilo na leo wanacheza mechi yao ya mwisho dhidi ya Gor kuanzia Saa 8:00 mchana.
    Khartoum N na Gor Mahia zote zina pointi saba kila moja baada ya kushinda mechi mbili mbili na kutoa sare moja katika mechi baina yao, wakati Yanga SC ni ya tatu kwa pointi zake sita za ushindi wa mechi mbili.
    Mshindi wa kwanza wa Kundi A atakutana na Malakia ya Sudan Kusini katika Robo Fainali, mshindi wa pili atakutana na Azam FC wakati mshindi wa tatu atakutana na APR ya Rwanda.
    Ikiwa sasa inashika nafasi ya tatu, Yanga SC ikifanikiwa kuifunga Khartoum N leo, inaweza ikapanda kileleni iwapo, Telecom watamudu hata kulazimisha sare na Gor Mahia, jambo ambalo halitarajiwi. Matarajio ni Gor kushinda, tena ushindi mnono.
    Na Yanga SC kuifunga Khartoum N si jambo jepesi pia, kwani timu hiyo inayofundishwa na Mghana Kwesi Appiah imeonyesha ubora wa soka yake katika mechi zilizotangulia.
    Yanga SC ikiongoza kundi, itacheza na Malakia, ikiwa ya pili itacheza na Azam FC na ikiwa ya tatu itakutana na APR, je itaangukia wapi?
    Dakika 180 za mechi mbili za leo (Gor Mahia Vs Telecom na Yanga SC Vs Khartoum N) ndiyo zitatoa majibu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam- ila mechi ya Yanga na Azam FC inanukia Robo Kagame 2015. 
    Mshambuliaji hatari wa Azam FC, Kipre Tchetche jana amefunga mabao mawili katika ushindi wa 5-0 dhidi ya Adama City

    Donald Ngoma amekuwa tishio kwa mabeki wa timu pinzani Kombe la Kagame akiwa na Yanga SC 

    MISIMAMO YA MAKUNDI KOMBE LA KAGAME

    Kundi A



    PWDLGFGAGDPts
    1Khartoum (Sudan)32107167
    2Gor Mahia (Kenya)32106337
    3Yanga (Tanzania)32016246
    4Telecom (Djibouti)300329-90

    Kundi B



    PWDLGFGAGDPts
    1APR (Rwanda)33005149
    2Al Shandy (Sudan)31115504
    3LLB (Burundi)302134-12
    4Heegan (Somalia)301225-3
    1

    Kundi C



    PWDLGFGAGDPts
    1Azam (Tanzania)33008089
    2KCCA (Uganda)32012116
    3Malakia (S. Kusini)310224-23
    4Adama (Ethiopia)300318-70



    Ratiba ya Kombe la Kagame

    Jumanne Julai 28, 2015
    APR vYanga/Gor/KhartoumSaa 8:00 Mchana
    Yanga/Gor/Khartoum
    vMalakiaSaa 10:00 Jioni
    Jumatano Julai 29, 2015


    Al ShandyvKCCASaa 8:00 Mchana
    Azam FCv
    Yanga/Gor/Khartoum
    10:00 Jioni

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MECHI YA YANGA NA AZAM FC YANUKIA ROBO FAINALI KAGAME 2015, ITAKUWA JUMATANO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top