Na Princess Asiaa, DAR ES SALAAAM
TIMU ya Chole United imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Mwezi Mtukufu wa Ramadhani baada ya kuifunga mabao 2-1 Saggar katika fainali usiku wa kuamia jana Uwanja wa shule ya Diamond, Upanga, Dar es Salaam.
Katika mchezo huo ambao mgeni rasmi alikuwa Diwani wa Upanga Mashariki (CCM), Sultan Ahmed Salim, shujaa wa mechi alikuwa ni Abaly mfungaji wa mabao yote ya Chole moja kila kipindi.
Chole United ambayo iliingia baada ya kuwafunga ndugu zao Chole Rangers kwa bahati, baada sare hadi kwenye penalti, kufuatia sare ya 2-2 Jumatatu, pia imetoa mfungaji bora wa mashindano, Lutfy Bin Kleb aliyefunga mabao manne sawa na Mohammed Sadat.
Saggar iliyoitoa DFC United kwa bao 1-0 katika Nusu Fainali, ilishindwa kufurukuta mbele ya Chole United iliyoongozwa na Nahodha Moudy Mass.
Wafadhili wa Chole, Abdallah Bin Kleb na Big Bon wamempongeza Lutfy kwa kuwa alicheza mechi zote kama beki wa kushoto, lakini bado akaweza kuwa mfungaji bora.
TIMU ya Chole United imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Mwezi Mtukufu wa Ramadhani baada ya kuifunga mabao 2-1 Saggar katika fainali usiku wa kuamia jana Uwanja wa shule ya Diamond, Upanga, Dar es Salaam.
Katika mchezo huo ambao mgeni rasmi alikuwa Diwani wa Upanga Mashariki (CCM), Sultan Ahmed Salim, shujaa wa mechi alikuwa ni Abaly mfungaji wa mabao yote ya Chole moja kila kipindi.
![]() |
| Nahodha wa Chole United, Moudy Mass akiinua Kombe la ubingwa wa mashindano ya mwezi mtukufu usiku wa kuamkia jana Uwanja wa shule ya Diamond, Upanga, Dar es Salaam, baada ya kuifunga Saggar 2-1 |
![]() |
| Washindi wakiwa na Kombe na Medali zao baada ya mechi |
Chole United ambayo iliingia baada ya kuwafunga ndugu zao Chole Rangers kwa bahati, baada sare hadi kwenye penalti, kufuatia sare ya 2-2 Jumatatu, pia imetoa mfungaji bora wa mashindano, Lutfy Bin Kleb aliyefunga mabao manne sawa na Mohammed Sadat.
Saggar iliyoitoa DFC United kwa bao 1-0 katika Nusu Fainali, ilishindwa kufurukuta mbele ya Chole United iliyoongozwa na Nahodha Moudy Mass.
Wafadhili wa Chole, Abdallah Bin Kleb na Big Bon wamempongeza Lutfy kwa kuwa alicheza mechi zote kama beki wa kushoto, lakini bado akaweza kuwa mfungaji bora.
![]() |
| Mabingwa; Kikosi cha Chole United kilichotwaa Kombe la Mwezi Mtukufu wa Ramadhani |
![]() |
| Lutfy (kushoto) akipongezwa na kaka yake, Abdallah Bin Kleb ambaye pia ni mmoja wa wafadhili wa Chole pamoja na Big Bon |
![]() |
| Wachezaji wa Chole wakishereheea na mashabiki wao baada ya ubingwa |
![]() |
| Mgeni rasmi akikabidhi Medali kwa washindi |








.png)
0 comments:
Post a Comment