KIUNGO James Milner ametambulishwa kama mchezaji wa Liverpool leo na kusema kiu yake ni kushinda mataji na Medali kibao akicheza dimba la kati Anfield.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa England amesema anataka kuendeleza desturi ya kuinua mataji kama ilivyokuwa Manchester City baada ya kupata nafasi ya kufanya kazi na kocha Brendan Rodgers.
Ingawa hakusema moja kwa moja kuhusu Steven Gerrard baada ya kukabidhiwa jezi namba 7, Milner alisema pengo lililoachwa na gwiji wa Liverpool halitasumbua.
James Milner ametambulishwa leo Liverpool na kusema anataka kushinda mataji na Medali Anfield
Kiungo huyo wa kimataifa wa England amepewa jezi namba 7 Liverpool baada ya kusajiliwa kutoka Manchester City PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment