IMEWEKWA AGOSTI 19, 2013 SAA 4:50 ASUBUHI
MWANASOKA bora wa dunia, Lionel Messi jana alifunga mabao mawili na kutengeneza lingine kuwasaidia Neymar na kocha wa Barcelona, Gerardo Martino kuanza kazi vizuri kwa ushindi wa 7-0 dhidi ya Levante kwenye Ligi Kuu ya Hispania.
Katika mchezo huo ambao Neymar alianzia benchi, mabao ya Barca yalifungwa na Sanchez dakika ya tatu, Messi dakika ya 12 na 42 kwa penalti, Alves dakika ya 23, Pedro dakika ya 26 na 73 na Xavi dakika ya 45.
Kikosi cha Barcelona kilikuwa: Valdés, Alves, Piqué, Mascherano, Adriano, Fàbregas, Busquests, Xavi, Pedro/Tello, Alexis/Neymar, Messi/Iniesta.
Levante: Navas, Navarro, Rodas, Barral, El Zhar, Rubén, Juanfran, Xumetra, Sergio, Pedro López na Simao.
Running riot: Lionel Messi and Co were lethal in the first match of the La Liga season, scoring six first half goals
Watching on: £50m wonderkid Neymar started the match from the bench
Big entrance: Neymar was a second half substitute but Barca had already taken their foot well off the gas by then
In action: Neymar wasn't able to get on the score sheet
Nayo Real Madrid imeanza vyema mbio zake za La Liga kwa ushindi mwembamba wa 2-1 dhidi ya Real Betis.
Jorge Molina aliwatuliza mashabiki Uwanja wa Bernabeu kwa bao la dakika ya 15, kabla ya Karim Benzema kusawazisha dakika 10 baadaye na mchezaji mpya, Isco akafunga la ushindi dakika ya 86.
Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Lopez, Pepe, Ramos, Khedira/Casemiro, Ronaldo, Benzema/Morata, Özil/Di Maria, Marcelo, Carvajal, Modric na Isco.
Real Betis: Andersen, Chica, Perquis, Paulao, Nacho, Matilla, Nosa, Verdú, Juanfran, Cedrick na Molina.
Shujaa: Isco ameifungia bao la ushindi dakika za lala salama Real Madrid
Ametoka kapa: Cristiano Ronaldo alipata nafasi kadhaa za kufunga, lakini akapoteza