• HABARI MPYA

    Monday, July 22, 2013

    ROONEY WA KAZI GANI KAMA SHUGHULI YENYEWE NI HII YA LUKAKU, HATA TORRES NA BA WACHUNGE SANA

    IMEWEKWA JULAI 22, 2013 SAA 7:51 USIKU
    HAIJALISHI hata kama Wayne Rooney hatopatikana, inaonekana Fernando Torres atakabiliana na ushindani mkali kutoka kwa Romelu Lukaku.
    Mshambuliaji huyo wa Ubelgiji anaendelea vizuri, akifunga kwa mara ya pili katika mechi mbili za kujiandaa na msimu, Chelsea ikiichapa Malaysia XI mabao 4-1 jana, na Jose Mourinho amesema hatahofia kuanza msimu na Lukaku akiongoza safu ya ushambuliaji.
    "Ni hivyo," alisema Mourinho, alipoulizwa kama kweli atashindana na Torres na Demba Ba, ambaye alichukua nafasi ya Lukaku mapumziko mjini Kuala Lumpur. 
    Next main man? Romelu Lukaku has impressed Jose Mourinho in Chelsea's pre-season friendlies, so much so he could be set to start up front for the opening fixtures of the Premier League season
    Kiongozi wa safu ya ushambuliaji ajaye? Romelu Lukaku amemvutia Jose Mourinho katika mechi za Chelsea kujiandaa na msimu.

    Lukaku anafanana mno kiuchezaji na shujaa wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba awali Mourinho alipokuwa Chelsea, hivyo anamvutia sana kocha wake na anaweza kuongoza safu katika Ligi Kuu.
    Torres hawezi kuwa na Mourinho tayari amekwishasema Mspanyola huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 50 hana madhara anapibanwa na hakuna nafasi ya kushambulia nyuma ya mabeki.
    Role model: Lukaku is an imposing centre forward, just like ex-Blues legend Dider Drogba (right)
    Role model: Lukaku is an imposing centre forward, just like ex-Blues legend Dider Drogba (right)
    Mfano wa kuigwa: Lukaku ni mshambuliaji hatari, kama alivyokuwa gwiji wa zamani wa Blues, Dider Drogba (kulia)
    Tough man to impress: Jose Mourinho has been delighted by Lukaku's progress
    Mtu wa nguvu wa kuvutia: Jose Mourinho amefurahishwa na maendeleo ya Lukaku

    Pamoja na hayo, Lukaku ana umri wa miaka 20 tu na Mourinho anaridhika kumbebesha mzigo huo tena kwa matarajio: "Tunatakiwa kumuheshimu Didier, kwa sababu ni wa kipekee katika historia ya Chelsea na tunatakiwa kumuheshimu Lukaku,"alisema kocha huyo.
    "Kitu kizuri kufanya ni kwamba kutomfananisha na gwiji katika historia ya Chelsea. Muache Didier huko alipo, katika kiwango cha juu cha historia ya Chelsea, na muache Lukaku ajitume. Kijana ni mzuri,".
    Ba ataanza Alhamisi katika mchezo wa mwisho wa ziara ya Asia dhidi ya Indonesia XI. Torres bado hajajiunga na kikosi akiendelea na mapumziko baada ya Kombe la Mabara.
    Chelsea ilipata pigo la majeruhi pamoja na kushinda Malaysia, baada ya Kevin de Bruyne kutolewa nje kufuatia kuumia goti lake la kuli, akifunga bao la pili usiku huo.
    De Bruyne, mwingine kati ya waliovutia katika ziara hiyo, aliondoka uwanjani akiwa ameshika mikono kichwani, ingawa taarifa za daktari zilisema hayatakuwa maumivu makubwa.
    Competition: Lukaku's emergence is bad news for strikers Demba Ba (left) and Fernando Torres (right)
    Competition: Lukaku's emergence is bad news for strikers Demba Ba (left) and Fernando Torres (right)
    Ushindani: Kuchanganya kwa Lukaku ni habari mbaya kwa washambuliaji Demba Ba (kushoto) na Fernando Torres (kulia)
    Unfortunate: Belgian midfielder Kevin de Bruyne's fine right footed finish resulted in him colliding with the defender and he was subsequently stretchered off the field
    Bahati mbaya: Kiungo Mbelgiji, Kevin de Bruyne akitolewa nje baada ya kuumia
    Impressive: Frontman Lukaku congratulates 17-year-old trialist Traore, who caught the eye in Asia
    Lukaku akipongezwa na kinda wa miaka 17 aliye majaribio, Traore, ambaye ameng'ara Asia

    Winga huyo Mbelgiji alifunga bao la kwanza kabla ya Bertrand Traore kufunga la pili, Lukaku la tatu na Victor Moses la nne, kabla ya Malaysia kupata la kufutia machozi. 
    Kiungo Traore ana miaka 17 tu na tayari ni mchezaji wa timu ya taifa ya Burkina Faso ambaye yupo kwenye majaribio kwa sababu ya viza ya mwanafunzi na hawezi kusaini Mkataba hadi atimize miaka 18 Septemba na hawezi kuomba kibali cha kufanya kazi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ROONEY WA KAZI GANI KAMA SHUGHULI YENYEWE NI HII YA LUKAKU, HATA TORRES NA BA WACHUNGE SANA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top