• HABARI MPYA

    Sunday, July 21, 2013

    MAJANGA ARSENAL, KOSCIENLY, SZCZESNY NA GIROUD WAUMIA MAZOEZINI NAGOYA

    IMEWEKWA JULAI 21, 2013 SAA 2:37 USIKU
    KOCHA Arsene Wenger amepata pigo tena katika safu yake ya ulinzi leo, baada ya Laurent Koscielny kugongana na kipa Wojciech Szczesny mazoezini na kuumia, hivyo ataukosa mchezo wa kirafiki kesho mjini Nagoya.
    Beki Mfaransa, Koscielny alitoka kwenye mazoezi mwishoni akionekana kama aliyeumia kifundo cha mguu wa kulia.
    Mara moja alitazamwa na dawati la tiba la The Gunners juu ya maumivu yake, kabla ya kupelekwa Uwanja wa Rugby wa Mizuno kwa uchunguzi zaidi.
    Larking about: Laurent Koscielny was in high spirits in Sunday's training session before picking up a knock
    Laurent Koscielny alikuwa na morali ya hali ya juu katika mazoezi ya leo kabla ya kuumia
    Popular: Theo Walcott signs autographs for the baying fans in Nagoya
    Theo Walcott akisaini autographs kwa mashabiki Nagoya
    Arsene Wenger
    Arsene Wenger
    Arsene Wenger akizungumza na mashabiki wakati wa mazoezi

    Ukubwa wa maumivu yaked bado haujajulikana, lakini anaonekana hatacheza mechi ya kesho.
    Benchi la Ufundi la Arsenal litafuatilia tatizo kwa saa 24, lakini wanaamini halitakuwa tatizo la muda mrefu.
    Na katika pigo lingine, Szczesny naye anaweza kuukosa mchezo wa kesho kutokana na maumivu.
    Crowd control: Security guards hold back the fans as they await the stars' arrival
    Walinzi wakiwadhibiti mashabiki waliokuwa wanasubiri nyota wa Arsenal wawasili
    Sign here: Bacary Sagna makes his way through the crowd before Arsenal's training session
    Saini hapa: Bacary Sagna akipasua katika ya umri ya mashabiki wakati Arsenal inakwenda kufanya mazoezi
    Warming up: The Arsenal squad warm up before a training session in Japan
    Kikosi cha TArsenal kikipasha nchini Japan
    Happy to be here: England duo Alex Oxlade-Chamberlain and Theo Walcott pose for a photo during training
    Furaha kuwa hapa: Wachezaji wa England, Alex Oxlade-Chamberlain na Theo Walcott wakipozi kwa picha wakati wa mazoezi

    Mpland huyo inafahamika aliumia mazoezini tangu wawasili Japan Ijumaa asubuhi.
    Aisha, Lukasz Fabianski au Damien Martinez mmojawapo atachukua nafasi ya Szczesny dhidi ya Nagoya Grampus.
    Habari za kuumia kwa Koscielny zinamaanisha Wenger ambaye kwa sasa tayari anamkosa beki wake mmoja mzoefu, Per Mertesacker katika ziara hii ya Mashariki ya Mbali; atamtumia kinda Ignasi Miquel kikosini.
    Wenger tayari anamkosa Thomas Vermaelen, ambaye yuko nje kwa miezi mitatu kwa majeruhi.
    Popular figure: Walcott has a fair few autographs to get through before he can get into training
    Walcott akisaini autographs kabla ya kuingia mazoezini
    All smiles: Lukas Podolski poses for the cameras from the team bus
    Lukas Podolski akipozi kwa ajili ya kamera akiwa ndani ya basi la timu
    Happy snapper: Podolski turns photographer during a training session in Japan
    Mpiga picha: Podolski aligeuka mpiga picha wakati wa mazoezi Japan
    Watching on: Per Mertesacker during a training session in Japan
    Per Mertesacker mazoezini Japan

    Maumivu ya Koscielny yanaweza kumfanya Wenger aharakishe jitihada za kumsajili sentahafu wa Swansea, Ashley Williams anayemuwania kwa muda mrefu.
    Mshambuliaji Olivier Giroud, ambaye ni mfungaji bora wa klabu katika mechi hizi za kujiandaa na msimu, akifunga mabao matano katika mechi mbili, pia aliumia mazoezini, lakini akainuka na kuendelea.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MAJANGA ARSENAL, KOSCIENLY, SZCZESNY NA GIROUD WAUMIA MAZOEZINI NAGOYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top