IMEWEKWA JULAI 23, 2013 SAA 12:14 JIONI
MAISHA si mepesi kwa David Moyes bara la Asia. Siyo tu kocha huyo mpya wa Manchester United anavyosotea saini ya kiungo wa Barcelona, Cesc Fabregas, timu yake sasa imepoteza mechi ya pili kati ya tatu za ziara ya kujiandaa na msimu.
Mchezo huo ulikuwa mgumu kuliko wa Jumamosi dhidi ya A-League All-Stars mjini Sydney na Manchester United imefungwa mabao 3-2 na Yokohama nchini Japan.
Baada ya kutanguliwa kwa bao la mapema sekunde ya 27, United ilipigana kiume na kufanikiwa kuongoza kwa mabao 2-1 hadi mapumziko baada ya Jess Lingard kusawazisha dakika ya 19 na beki wa Marinos, Masakazu Tashiro kujifunga dakika ya 31.

Marquinhos akifunga bao la kwanza sekunde ya 27

Jesse Lingard (kulia) amekuwa katika kiwango kizuri na ameifungia bao United leo
Kikosi cha Man United kilikuwa: De Gea; Fabio, Jones, Evans/Smalling, Evra, Anderson, Cleverley, Zaha/Giggs, Lingard/Ashley Young, Januzaj/Kagawa na Van Persie/Welbeck.Lakini timu ya Japanese ikasawazisha haraka kipindi cha pili na ikapata bao la ushindi zikiwa zimesalia dakika tatu, wakati Yoshihito Fujita aliyetokea benchi alipomtungua David de Gea kutoka umbali wa mita 12, baada ya Jin Hanato kuwatoka Patrice Evra na Phil Jones upande wa kushoto.
Yokohama: Enomoto, Dutra, Aguiar, Tashiro, Kobayahsi, Nakamura, Hyodo, Tomisawa, Nakamachi, Marquinhos na Sato.

Robin van Persie akijaribu kumtoka beki wa Yokohama Marinos, Masakazu Tashiro

Van Persie akipiga mpira mbele ya beki wa Kijapan, Yuzo Kobayashi

Kinda wa United, Adnan Januzaj akigombea mpira na Dutra

Mashabiki wawili wa wakimsapoti Shinji Kagawa na Robin van Persie

Wilfried Zaha yuko vizuri

Shinji Kagawa alikuwa kivutio

David Moyes akimuangalia Danny Welbeck akirusha mpira

Lingard akifunga badaa ya kazi nzuri ya Wilfried Zaha

Shinji Kagawa (kushoto) aling'ara akicheza nyumbani

Danny Welbeck akipambana

Wajeshi Wekundu: Mashabiki watoto wa United

Mashabiki wa Japan wakiwa wamevaa jezi ya nyota wa United, Kagawa

Nyota wa Japan, Kagawa anapendwa mno nyumbani


.png)