• HABARI MPYA

    Thursday, March 22, 2012

    MANCINI SASA AYASEMA YOTE KWA TEVEZ


    Manchini kulia na Tevez
    KOCHA wa Manchester City, Roberto Mancini anatarajia Carlos Tevez atasaidia sana klabu yake kutimiza ndoto za kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England baada ya kuanza kazi rasmi jana.
    Tevez alikuwa kivutia kwenye ushindi wa 2-1 dhidi ya Chelsea akirejea kwa mara ya kwanza tangu Septemba usiku wa jana Uwanja wa Eastlands, ingawa alianzia benchi.
    Mshambuliaji huyo wa Argentina alimsetia bao la ushindi Samir Nasri na kuifanya timu yake ipunguze pengo la pointi hadi kubaki moja dhidi ya vinara wa ligi hiyo, Manchester United.
    Sergio Aguero alisawazisha kwa penalti dakika chache tu baada ya Tevez kuingia hivyo kufanya mchezo uwe 1-1 baada ya Gary Cahill kutangulia kuifungia Chelsea.
    "Nafikiri kwamba ilikuwa muhimu Carlos alitoa pasi nzuri kwa Samir kufunga na mashabiki wote walifurahia hilo," alisema Mancini.
    "Nafikiri Carlos anahitaji muda zaidi, si kazi nyepesi kwake, lakini ni muhimu kwamba yupo hapa sasa.
    "Labda ndani ya siku 10, wiki mbili, atakuwa kwenye kiwango kizuri. Nafikiri kwamba itakuwa muhimu kwetu.
    "Carlos anaweza asiwe katika kiwango chake kwa asilimia 100, lakini anafahamu soka na alikuwa muhimu kwa sababu alitufanyia jambo kubwa.
    "Nimekuwa nikizungumza na Carlos kila siku mwezi huu na anafahamu alitakiwa kutokea benchi na kucheza dakika 20 katika mchezo huo, lakini anaweza kucheza zaidi.
    "Ni mchezaji muhimu, anahitaji wiki nyingine mbili au tatu kuwa katika kiwangokizuri, lakini wakati anacheza, anajua wapi pa kupeleka mpira."
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MANCINI SASA AYASEMA YOTE KWA TEVEZ Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top