• HABARI MPYA

    Wednesday, March 28, 2012

    ALGERIA MABINGWA U-17 KASKAZINI


    TIMU ya taifa ya Algeria imetwaa ubingwa wa Afrika Kaskazini kwa vijana chini ya umri wa miaka 17, (UNAF) iliyomalizika mjini Kalaa Kebira, Tunisia wiki iliyopita.
    Junior Desert Foxes walitwaa taji hilo baada ya kutoa sare na wenyeji Tunisia kwenye michuano hiyo iliyoanza Machi 20 hadi 24.
    Algeria ilivuna pointi nyingi zaidi kwenye michuano hiyo iliyochezwa kwa mtindo wa mzunguko, Mauritania ikiwa timu nyingine iliyoshiriki.
    Algeria, washindi wa michuano iliyopita, walimaliza wakiwa na pointi nne, Mauritania tatu na Tunisia pointi moja.
    Wakati huo huo: Michuano ijayo ya UNAF U-17 itafanyika Dar El-Beida kuanzia Machi 27 hadi 30, washiriki wakiwa wenyeji Algeria, Mauritania, Morocco na Tunisia.

    MATOKEO UNAF U-17:
    Siku ya kwanza:
    Algeria 2-0 Mauritania
    Siku ya Pili
    Tunisia 1-2 Mauritania
    Siku ya Tatu
    Algeria 0-0 Tunisia

    MSIMAMO WAKE:
                           P   W   D   L   GF  GA  GD  Pts
    Algeria             2   1    1   0    2    0   +2    4
    Mauritania        2   1    0   1    2    3   -1     3
    Tunisia             2   0    1   1    1    2   -1     1
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ALGERIA MABINGWA U-17 KASKAZINI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top