• HABARI MPYA

    Wednesday, March 28, 2012

    REFA AWAPA WATANO KADI NYEKUNDU CHUMBANI

    Kocha wa Bradford
    REFA aliwapa kadi nyekundu wachezaji watano katika chumba cha kubadilishia nguo baada ya mechi ya Ligi Daraja la Nne England, League Two kati ya Bradford City na Crawley Town.
    "Siwezi kuamini kilichotokea," alisema kocha wa Bradford, Phil Parkinson, ambaye awali wachezaji wake watatu walipewa kadi nyekundu jana katika mechi hiyo, ambayo walifungwa 2-1 nyumbani.
    "Sijawahi kukutana na mazingira kama haya, refa anakuja chumba cha kubadilishia nguo, anawaweka wachezaji upande mmoja na kuwapa kadi nyekundu. Hakuniruhusu kufanya chochote pale."
    Wachezaji sita wa Crawley na mmoja wa Bradford walipewa kadi za njano katika mechi hiyo, Andrew Davies wa Bradford, ambaye alipewa kadi nyekundu, sasa anajiandaa kutumikia adhabu ya kukosa mechi tano baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu mara mbili awali msimu huu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REFA AWAPA WATANO KADI NYEKUNDU CHUMBANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top