• HABARI MPYA

    Thursday, March 22, 2012

    MCHEZAJI INDIA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKA UWANJANI, NI KAMA ISHU YA MUAMBA TU


    MWANASOKA wa India, amefariki dunia baada ya kuzimia uwanjani katika mechi ya ligi ya nyumbani kusini mwa jiji la Bangalore.
    D. Venkatesh akiwa na umri wa miaka 27, kiungo wa klabu ya Daraja la A, Bangalore Mars, aliingia uwanjani akitokea benchi dakika ya 73 na akazimia mwishoni mwa mchezo, imesema taarifa ya madaktari nchini humo leo.
    Vyombo vya habari vya nchini humo vilisema hakukuwa na gari la wagonjwa na Venkatesh alipelekwa hosptali ya Hosmat Jumatano kwa bajaji.
    Taarifa za awali zinasema kwamba uzembe ulichangia kifo chake.
    Kifo cha Venkatesh kinakuja siku tatu baada ya kiungo wa Bolton, Fabrice Muamba kuanguka na kuzimia katika mechi ya Kombe la FA England akiichezea timu yake dhidi ya Tottenham. Lakini Muamba alinusurika kwa sababu aliwahi kupelekwa hospitali ya London Chest ambako bado anaendelea na tiba yakinifu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MCHEZAJI INDIA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKA UWANJANI, NI KAMA ISHU YA MUAMBA TU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top