• HABARI MPYA

    Tuesday, March 27, 2012

    BEKI LA SENEGAL MIEZI MITATU KITANDANI

    Diawarra
    BEKI wa Olympique Marseille, Souleymane Diawara atakwenda kufanyiwa upasuaji wa goti zoezi ambalo litamfanya awe nje ya Uwanja kwa miezi sita, imesema klabu yake Ligi Kuu Ufaransa, Ligue 1 jana.
    Beki huyo wa kati wa Senegal, Diawara aliuamia vibaya goti lake la kulia hadi kutoa machozi Jumamosi, timu yake ikitoka 1-1  na Nice.
    “Atakwenda kufanyiwa upasuaji wiki ijayo. Atakuwa nje ya Uwanja kwa kiasi cha miezi sita,” ilisema Marseille katika tovuti yake.
    Diawara ataikosa sehemu yote ya msimu iliyobaki na atakuwa tayari kuanza tena kazi wakati msimu ujao unaanza Agosti.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BEKI LA SENEGAL MIEZI MITATU KITANDANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top