BAO la Jamie Mackie liliipa ushindi QPR ikitokea nyuma
zikiwa zimebaki dakika 13 na kuifunga Liverpool hivyo kufanikiwa kujiondoa
kwenye eneo la hatari ya kushuka daraja.
Sebastian Coates alianza na kufunga na Dirk Kuyt akawafungia
Wekundu wa Anfield na kuwaweka mbele kwenye mchezo huo.
Shaun Derry alirejesha matumaini QPR hkwa bao la kichwa
kabla ya mchezaji wa zamani wa Wekundu hao, Djibril Cisse kuwarudi kwa kuwafunga
na kufanya 2-2.
Kosa la Jose Enrique lilimpa nafasi Mackie kufunga bao la
ushindi dakika za majeruhi akimtungua kipa Pepe Reina kuipatia bao la ushindi QPR.
Kipigo hicho kinaiacha Liverpool iwe na matumaini finyu ya
kumaliza ndani ya timu za nne za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu England, huku
Wekundu hao wakiwa wanazidiwa pointi 12 na Tottenham wanaoshika nafasi ya nne,
baada ya kipigo hicho cha nne kwenye mechi tano za ligi.
Katika mchezo mwingine, Arsenal ilishinda 1-0 ugenini dhidi
ya Everton na Tottenham Hotspur ililazimishwa sare ya 1-1 na Stoke City.



.png)
0 comments:
Post a Comment