• HABARI MPYA

    Friday, March 23, 2012

    LIVERPOOL HAWAJUI CHA KUFANYA NA TIMU LA DALGLISH


    Dalglish
    WAKATI Liverpool kesho inaingia kwenye mchezo mwingine wa Ligi Kuu ya England dhidi ya timu iliyo kwenye hatari ya kushuka daraja, Wigan kwenye Uwanja wa Anfield, mashabiki wa timu hiyo hawajui cha kufanya kwa kikosi cha kocha, Kenny Dalglish.
    Dalglish ameleta Kombe la kwanza tangu mwaka 2006 kwa kuifunga Cardiff kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Wekundu hao watakutana na ama Everton au Sunderland kwenye Nusu Fainali ya Kombe la FA mwezi ujao.
    Lakini mwenendo wa Liverpool katika ligi msimu wote umekuwa mbovu na kipigo cha mabao 3-2 walichokipata kutoka kwa QPR – wakati walikuwa wanaongoza 2-0 katikati ya wiki kilikuwa ni cha tisa msimu huu katika mechi 29.
    Wamefungwa mechi nane kati ya 15 za ugenini na rekodi yao mbele ya mashabiki wao pia inakanganya.
    Timu ya Dalglish imefungwa mara moja tu nyumbani, 2-1 na Arsenal mwanzoni mwa msimu, lakini wamemudu kushinda mechi tano tu dhidi ya Norwich, Swansea, Blackburn na Stoke ni miongoni mwa timu nane zilizoondoka na sare Anfield.
    Hiyo inawafanya wazidiwe pointi 28 na vinara wa Ligi Kuu, Manchester United ambao ni wapinzani wao wakubwa na wanaizidi pointi 19 Bolton inayoshika nafasi ya tatu kutoka mkiani.
    Akiwa ametumia kiasi cha pauni Milioni 110 tangu arejee Anfield Januari, mwaka jana, Dalglish alitarajia mambo makubwa kutokana na uwekezaji wake.
    Baada ya mechi ya QPR, kocha huyo wa Liverpool alisema; "Tunahitaji kutafuta maswali na kuhakikisha tunakwenda kujifunza kutokana na hili, tulitawala sehemu kubwa ya mchezo, mipango na uwezo, lakini (QPR) wameondoka na pointi tatu."alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL HAWAJUI CHA KUFANYA NA TIMU LA DALGLISH Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top