• HABARI MPYA

    Friday, March 23, 2012

    ARSENAL WAPANIA KUWAPOTEZA KABISA SPURS


    Laurent Koscielny 
    WASHIKA Bundi wa London watataka kuonyesha dhamira yao ya kumaliza ndani ya tatu bora katika msimamo wa Ligi Kuu ya England kwa kushinda nyumbani dhidi ya Aston Villa kesho.
    Ushindi wa nyumbani Jumatano 1-0 dhidi ya Everton umewafanya vijana wa Arsene Wenger, waliokuwa wanazidiwa pointi 10 wiki kadhaa zilizopita, kupanda juu ya wapinzani wao katika jiji la London, Tottenham Hotspur, ambao walilazimishwa sare na toke.
    Tottenham watarejea juu iwapo wataifunga Chelsea kwa mara ya kwanza tangu 1990 kesho, lakini ushindi wa nyumbani Uwanja wa Emirates, dhidi ya wapinzani walio katika nafasi ya 15, utawarejesha Arsenal juu tena.
    Ushindi dhidi ya Everton ulikuwa wa sita mfululizo kwa Arsenal katika Ligi Kuu na pia ulikuwa wa kwanza kushinda bila ya nyavu zao kuguswa kwenye michuano hiyo tangu Februari.
    Wenger alianza vibaya msimu huu kutokana na kuwa na majeruhi wengi, jambo ambalo lilimgharimu kupigwa mabao 8-2 na Manchester United Agosti.
    Baadhi walikwishaanza kumshutumu Mfaransa huyo kwa kuwa mtu wa kuomba sana msamaha, lakini kurejea kwa mabeki wake tegemeo kumekuwa chachu ya mafanikio ya siku za karibuni kwa Arsenal.
    Thomas Vermaelen, aliyefunga bao pekee la ushindi dhidi ya Everton, alikosekana muda mrefu na amerejea vema wakati mabeki wa pembeni Bacary Sagna na Kieran Gibbs nao wameonyesha kurudi vizuri katika Ligi Kuu wiki za karibuni.
    Laurent Koscielny ameonyesha ni kifaa kingine muhimu kwa safu ya ulinzi ya Arsenal na sasa Mfaransa huyo amewataka wachezaji wenzake wa Arsenal kudumisha cheche zao.
    Per Mertesacker, Jack Wilshere na Emmanuel Frimpong wataendelea kuwa nje ya Uwanja kwa muda mrefu, lakini Abou Diaby alicheza kiasi cha saa katika kikosi cha wachezaji wa akiba na Liverpool Jumanne akitoka kwenye maumivu ya nyama.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL WAPANIA KUWAPOTEZA KABISA SPURS Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top