• HABARI MPYA

    Friday, March 23, 2012

    YANGA WAHAMIA KIGAMBONI


    Papic akiongoza mazoezi Yanga
    KLABU ya Yanga ya Dar es Salaam imehamia kwenye Uwanja wa Tiper, Kigamboni kwa ajili ya mazoezi ya kumalizia msimu huu wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
    Kocha wa Mserbia, Kostadin Bozidar Papic ameiambia bongostaz asubuhi hii kwamba leo ndio wanaanza rasmi kufanyia mazoezi kwenye Uwanja huo.
    Alipoulizwa sababu za kuhamia huko, kocha huyo wa zamani wa Orlando Pirates, Kaizer Chiefs na Meritzburg Classic za Afrika Kusini alisema lengo ni kupata sehemu itakayowafaa bila kuwaathiri wachezaji wao kwa namna yoyote.
    Yanga ipo kwenye vita ya kutetea ubingwa wake wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ikikabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa Simba SC inayoongoza na Azam inayoshika nafasi ya pili, wakati mabingwa hao watetezi wapo nafasi ya pili.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA WAHAMIA KIGAMBONI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top