• HABARI MPYA

    Friday, March 23, 2012

    AGUERO ASEMA MAN CITY HAWANA MCHECHE NA STOKE


    Aguero
    MSHAMBULIAJI Sergio Aguero amesema Manchester City hawana mchecheto kuelekea mechi yao na Stoke wakiwania kurejea kileleni mwa Ligi Kuu.
    Kikosi cha Tony Pulis, Stoke kimekuwa nma matokeo mazuri kwenye Uwanja wake wa Britannia tangu wapande Ligi Kuu mwaka 2008.
    City waliambulia pointi mbili tu katika mechi tatu za Ligi Kuu walizocheza Stoke na pia walitolewa na timu hiyo kwenye Kombe la FA mwaka 2010.
    Kikosi cha Roberto Mancini, pia kilifungwa kwenye mechi ya mwisho ugenini na Swansea na kupoteza usukani wa Ligi Kuu tangu Oktoba.
    Lakini walipunguza idadi ya pointi wanazozidiwa na vinara, Manchester United, ambao pia ni mabingwa watetezi na kubaki moja baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Chelsea katikati ya wiki.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AGUERO ASEMA MAN CITY HAWANA MCHECHE NA STOKE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top