• HABARI MPYA

    Friday, February 14, 2014

    KEOWN AMPANGIA BONGE LA KIKOSI MOYES MAN UNITED AKIKITUMIA NI USHINDI MWANZO MWISHO

    KOCHA David Moyes ametumia vikosi tofauti vya kwanza katika mechi zote 39 alizoiongoza Manchester United hadi sasa, lakini beki wa zamani wa Arsenal, Martin Keown ambaye kwa sasa anaandikia Daily Mail la Uingereza amempa ushauri wa bure.
    Keown ameandika leo katika Daily Mail akimtaka Moyes kuacha kubadilisha vikosi na atumie kikosi cha kwanza kimoja tu, akiwaanzisha De Gea, Smalling, Evra, Valencia, Fletcher, Carrick, Mata, Rooney, Januzaj na Van Persie.
    Man United imekuwa na mwenendo mbaya chini ya Moyes aliyerithi mikoba ya Sir Alex Ferguson aliyejiuzulu mwishoni mwa msimu uliopita na sasa inaelekea tu si kutema ubingwa, bali kukosa hata nafasi ya kucheza michuano ya Ulaya mwakani.

    Stick with it! David Moyes needs to start playing a consistent team rather than chopping and changing
    Acha mapepe! David Moyes ameshauriwa kuacha kubadilisha vikosi Man United na atumie kikosi hicho hapo chini katika mechi zote.
    Best team: The starting XI that David Moyes should be playing when they are available

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KEOWN AMPANGIA BONGE LA KIKOSI MOYES MAN UNITED AKIKITUMIA NI USHINDI MWANZO MWISHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top