• HABARI MPYA

    Saturday, February 22, 2014

    MAN CITY YASHINDA 1-0 TU ETIHAD

    BAADA ya kuadhiriwa na Barcelona katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, Manchester City imerejea kwenye wimbi la ushindi baada ya kuilaza 1-0 Stoke City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Etihad usiku huu.
    City ilishindwa kufunga bao hata moja katika mechi zao tatu zilizopita kati ya nne na hadi mapumziko leo ilikuwa haijapata bao.
    Manuel Pellegrini akawaingiza Jeses Navas na Stevan Jovetic kipindi cha pili na hapo ndipo ilipopata ushindi, kufuatia bao la Yaya Toure dakika ya 70, ambalo linakuwa bao lake la 16 msimu huu.
    Matokeo hayo yanafanya City ibaki inazidiwa pointi tatu tu vinara wa Ligi Kuu Chelsea, ingawa kikosi cha Manuel Pellegrini kina mchezo mmoja mkononi.

    Kishindo cha furaha: Yaya Toure (juu) akimrukia Aleksander Kolorov mgongoni baada ya kufunga bao pekee la ushindi
    Twinkle toes: Toure (R) dances through the Stoke defence to open the scoring in the second half
    Toure (kulia) akiwatoka mabeki wa Stoke kabla ya kufunga
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN CITY YASHINDA 1-0 TU ETIHAD Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top